-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
Kwa miaka mingi ubongo wa mwanadamu umefananishwa na kompyuta, lakini mambo yaliyogunduliwa karibuni yanaonyesha kwamba ulinganifu wa ubongo na kompyuta haufai hata kidogo. “Mtu hata anawezaje kuanza kufahamu utendaji wa kiungo ambacho kina chembe za neva zipatazo bilioni 50 ambazo nazo zina miunganisho ipatayo bilioni milioni moja, na yenye utendaji wa ujumla wa labda bilioni milioni 10 kwa sekunde moja?” akauliza Dakt. Richard M. Restak. Yeye alijibuje? “Uwezo wa hata kompyuta za hali ya juu zaidi ambazo zinaiga utendaji wa ubongo . . . unashindwa na uwezo wa ubongo wa nzi kwa mara elfu kumi.” Basi, fikiria kadiri ambayo kompyuta inashindwa kufikia ubongo wa binadamu, ambao ni wa hali ya juu kabisa.
Ni kompyuta gani ambayo imetengenezwa na binadamu iwezayo kujirekebisha, ijiratibu yenyewe, au hata kujiboresha kadiri wakati upitavyo? Mfumo wa kompyuta unapohitaji kurekebishwa, ni lazima mtayarishaji wa programu aandike na kuingiza maagizo mapya katika mfumo huo. Ubongo wetu hufanya kazi hiyo peke yake, katika umri mchanga na vilevile katika umri wa uzee. Si kutia chumvi kusema kwamba kompyuta za hali ya juu zaidi ni bure sana kwa kulinganisha na ubongo. Wanasayansi wameuita ubongo “kitu tata zaidi kijulikanacho” na “kitu tata zaidi ulimwenguni.” Ebu fikiria baadhi ya ugunduzi ambao umefanya wengi wakate kauli ya kwamba ubongo wa binadamu umefanyizwa na Muumba mwenye kujali.
-
-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 51]
Bingwa wa Mchezo wa Chesi Dhidi ya Kompyuta
Wakati kompyuta ya hali ya juu iitwayo Deep Blue iliposhinda bingwa wa ulimwengu wa mchezo wa chesi, swali lilizushwa, “Je, hatulazimiki kukiri kwamba hiyo Deep Blue lazima iwe na akili?”
Profesa David Gelernter wa Chuo Kikuu cha Yale alijibu: “La. Deep Blue ni mashine tu. Haina akili kama vile chungu cha maua kisivyo na akili. . . . Jambo kuu ni hili: wanadamu ni bingwa wa kutengeneza mashine.”
Profesa Gelernter alitaja tofauti hii kubwa: “Ubongo ni mashine ambayo ina uwezo wa kukufanya ‘ujitambue.’ Ubongo unaweza kufanyiza picha akilini, na kompyuta haziwezi.”
Yeye alimalizia: “Pengo lililopo kati ya wanadamu na [kompyuta] ni la daima nalo haliwezi kuzibwa kamwe. Mashine zitaendelea kufanya maisha yawe rahisi, bora, yenye kupendeza na yenye kutatanisha zaidi. Na hatimaye, wanadamu wataendelea kushughulikia mambo yaleyale ambayo wao wamekuwa wakiyashughulikia: kujihusu, kuhusu mmoja na mwenzake na, wengi wao, kuhusu Mungu. Katika mambo haya, mashine hazijapata kutokeza tofauti. Nazo hazitaweza kamwe.”
-
-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 53]
Kompyuta Bora Zaidi Yatoshana na Konokono
“Kompyuta za leo hata hazifikii mwanadamu mwenye umri wa miaka 4 kwa uwezo wa kuona, kuzungumza, kusonga, au kutumia akili. Bila shaka sababu moja ni utendaji wa hali ya juu wa ubongo. Imekadiriwa kwamba uwezo wa kuchanganua habari wa hata kompyuta yenye nguvu zaidi unatoshana na uwezo wa mfumo wa neva wa konokono—sehemu kidogo sana ya uwezo wa ubongo wetu.”—Steven Pinker, mkurugenzi wa Kituo cha Sayansi ya Ufahamu na Ubongo katika Taasisi ya Tekinolojia ya Massachusetts.
-