Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Washikamanifu na Imara Zamani na Sasa
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
    • “Kukataa utumishi wa kijeshi kulimaanisha kupelekwa kwenye kambi ya mateso, labda Auschwitz,” asema Andrzej Szalbot aliyekamatwa na Gestapo mwaka wa 1943. “Sikuwa nimebatizwa bado, lakini nilijua uhakikisho ambao Yesu alitupatia kwenye Mathayo 10:28, 29. Nilijua kwamba nikifa kwa sababu ya imani yangu katika Yehova, ataweza kunifufua.”

      Mapema mwaka wa 1942, Wanazi waliwakamata ndugu 17 kutoka Wisła. Baada ya miezi mitatu, 15 kati yao walikufa huko Auschwitz. Mashahidi wengine waliobaki Wisła waliathiriwaje na jambo hilo? Badala ya kukana imani yao, jambo hilo liliwatia moyo washikamane na Yehova bila kulegea! Miezi sita iliyofuata, idadi ya wahubiri huko Wisła iliongezeka maradufu. Baada ya muda mfupi, wengi zaidi walikamatwa. Kwa ujumla, ndugu 83, watu wenye kupendezwa, na watoto waliathiriwa na kikosi chenye nguvu kilichotumiwa na Hitler. Kati yao, 53 walipelekwa kwenye kambi za mateso (hasa Auschwitz) au kwenye kambi za kazi ngumu katika migodi na machimbo huko Poland, Ujerumani, na Bohemia.

      Washikamanifu na Imara

      Huko Auschwitz, Wanazi walijaribu kuwashawishi Mashahidi kwamba watawapa uhuru mara moja. Askari mmoja wa SS alimwambia ndugu fulani hivi: “Ukitia tu sahihi hati ya kuonyesha kwamba umewakana Wanafunzi wa Biblia, tutakuachilia, nawe utaenda nyumbani.” Aliambiwa jambo hilo mara nyingi, lakini ndugu huyo aliendelea kuwa mwaminifu kwa Yehova. Kwa sababu hiyo, alipigwa, akadhihakiwa, na kupelekwa kwenye kambi za kazi ngumu huko Auschwitz na Mittelbau-Dora, Ujerumani. Kabla tu ya ukombozi, ndugu huyo aliponea chupuchupu kufa wakati kambi alimokuwa amezuiliwa ilipopigwa makombora.

      Paweł Szalbot, Shahidi aliyekufa hivi karibuni, alikumbuka hivi pindi moja: “Wakati wa kuhojiwa, askari wa Gestapo waliniuliza mara nyingi kwa nini sikujiunga na jeshi la Ujerumani na kukataa kusema Heil Hitler.” Baada ya kueleza msimamo wake wa Kikristo wa kutokuwamo akitumia Biblia, alipelekwa kufanya kazi katika kiwanda cha kutengeneza silaha. “Bila shaka, dhamiri yangu haingeniruhusu kufanya kazi hiyo, kwa hiyo walinipeleka nikafanye kazi kwenye mgodi.” Bado, aliendelea kuwa mwaminifu.

      Wale ambao hawakufungwa gerezani—wanawake na watoto—waliwatumia vifurushi vya chakula wale waliokuwa Auschwitz. “Wakati wa kiangazi tulichuma matunda madogo mekundu ya porini kisha tukayabadilisha kwa ngano,” asema ndugu mmoja aliyekuwa kijana wakati huo. “Akina dada walioka mikate na kuiloweka ndani ya mafuta. Kisha tukawapelekea waamini wenzetu waliokuwa gerezani mikate hiyo kwa kiasi kidogo-kidogo.”

  • Washikamanifu na Imara Zamani na Sasa
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
    • [Picha katika ukurasa wa 27]

      Akina ndugu walipotumwa na kufa huko Auschwitz, bado kazi iliendelea kukua huko Wisła

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki