11, 12. (a) Watu fulani wanaofanya dhambi nzito huzidisha tatizo lao kwa njia gani? (b) Ni uwongo gani unaoenezwa na Shetani kuhusu dhambi nzito, nasi tunaweza kuupinga jinsi gani? (c) Ni kwa njia gani tunaweza kuonyesha kwamba sisi ni wanyoofu kwa tengenezo la Yehova?
11 Ni muhimu tuwe wanyoofu hasa tunaposhughulika na wale wanaoongoza kutanikoni. Watu fulani wanaofanya dhambi nzito huzidisha tatizo lao kwa kujaribu kuficha dhambi yao na kudanganya wakati wazee wa kutaniko wanapowauliza. Watu hao hata huanza kuishi maisha ya unafiki, kwa upande mmoja wanajifanya wanamtumikia Yehova na wakati huohuo wanaendelea kutenda dhambi nzito. Hivyo, inaweza kusemwa kwamba watu hao wanaishi maisha ya uwongo. (Zaburi 12:2) Wengine wanawaambia wazee ukweli kwa kadiri fulani huku wakificha habari muhimu. (Matendo 5:1-11) Mara nyingi udanganyifu kama huo unatokana na kuamini uwongo ambao Shetani anaeneza.—Ona sanduku “Uwongo Ambao Shetani Anaeneza Kuhusu Dhambi Nzito.”