Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • 11, 12. (a) Watu fulani wanaofanya dhambi nzito huzidisha tatizo lao kwa njia gani? (b) Ni uwongo gani unaoenezwa na Shetani kuhusu dhambi nzito, nasi tunaweza kuupinga jinsi gani? (c) Ni kwa njia gani tunaweza kuonyesha kwamba sisi ni wanyoofu kwa tengenezo la Yehova?

      11 Ni muhimu tuwe wanyoofu hasa tunaposhughulika na wale wanaoongoza kutanikoni. Watu fulani wanaofanya dhambi nzito huzidisha tatizo lao kwa kujaribu kuficha dhambi yao na kudanganya wakati wazee wa kutaniko wanapowauliza. Watu hao hata huanza kuishi maisha ya unafiki, kwa upande mmoja wanajifanya wanamtumikia Yehova na wakati huohuo wanaendelea kutenda dhambi nzito. Hivyo, inaweza kusemwa kwamba watu hao wanaishi maisha ya uwongo. (Zaburi 12:2) Wengine wanawaambia wazee ukweli kwa kadiri fulani huku wakificha habari muhimu. (Matendo 5:1-11) Mara nyingi udanganyifu kama huo unatokana na kuamini uwongo ambao Shetani anaeneza.—Ona sanduku “Uwongo Ambao Shetani Anaeneza Kuhusu Dhambi Nzito.”

      UWONGO AMBAO SHETANI ANAENEZA KUHUSU DHAMBI NZITO

      Kuna uwongo hatari kuhusu dhambi nzito ambao Shetani angependa uamini. Lakini, Wakristo hawakosi kuzijua “hila” za Ibilisi. (Waefeso 6:11) Fikiria mambo matatu ya uwongo.

      • “Dhambi zinaweza kufichwa.” Ukweli ni kwamba Yehova anaona kila kitu tunachofanya. “Vitu vyote viko uchi navyo vimefunuliwa wazi machoni pake yeye ambaye tunatoa hesabu kwake.” (Waebrania 4:13) Kwa kuwa Yehova anajua ukweli wa mambo na tunawajibika kwake, kwa nini tujiongezee hatia kwa kujaribu kuwaficha watumishi wake wanadamu dhambi nzito?—Ona pia 2 Samweli 12:12.

      • “Wazee hawaaminiki, kwa hiyo usiwaambie chochote.” Mfalme Ahabu mwovu alimwita Eliya, “Ewe adui yangu.” (1 Wafalme 21:20) Kwa sababu alikuwa nabii wa Yehova katika Israeli, Eliya angeweza kumsaidia Ahabu kupata msamaha. Katika kutaniko la Kikristo, Yesu anaandaa wazee kuwa “zawadi katika wanadamu.” (Waefeso 4:8) Ingawa wao si wakamilifu, wazee “wanaendelea kuzilinda nafsi [zetu],” yaani, wanahangaikia afya na hali yetu ya kiroho. (Waebrania 13:17) Wao si adui zetu; wanatumiwa na Yehova kutusaidia.

      • “Kumsaidia rafiki kuficha dhambi ni kumlinda.” Ukweli ni kwamba tunaweza kumhatarisha mtenda-dhambi hata zaidi tunapomsaidia kuficha dhambi zake. Dhambi nzito ni dalili za ugonjwa hatari wa kiroho; kuzificha ni kama kumficha daktari mwenye ustadi dalili muhimu. (Yakobo 5:14, 15) Huenda mtenda-dhambi akaogopa kwamba atapokea nidhamu; lakini nidhamu inaonyesha kwamba Yehova anampenda, na inaweza kuokoa uhai wake. (Methali 3:12; 4:13) Zaidi ya hilo, mtu anayezoea kutenda dhambi anaweza kuwahatarisha wengine kutanikoni. Je, ungependa kufanya jambo ambalo litaeneza kutanikoni mitazamo yake mibaya iliyomwongoza kwenye dhambi? (Mambo ya Walawi 5:1; 1 Timotheo 5:22) Basi, hakikisha kwamba mkosaji amewaeleza wazee wa kutaniko kosa lake.

  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki