-
Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
huko Yerusalemu, karibu Machi 21 hivi. Kwa kawaida, kila mwaka mwadhimisho wa Ukumbusho huangukia tarehe ambayo mwezi mpevu huonekana kwa mara ya kwanza baada ya Machi 21.
30 Andiko la Mathayo 26:26-28 linataja maneno ya Yesu kuhusu jinsi Ukumbusho unavyopaswa kuadhimishwa. Ukumbusho si desturi yenye mafumbo, bali ni mlo wa mfano ambao unaliwa na wale waliochaguliwa kuwa warithi pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wake wa mbinguni. (Luka 22:28-30) Wakristo wengine wote waliojiweka wakfu na watu wanaopendezwa hutiwa moyo kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana wakiwa watazamaji. Wanapohudhuria, wanaonyesha kwamba wanathamini maandalizi ambayo Yehova Mungu amefanya kupitia Mwanaye, Yesu Kristo, kwa faida ya wanadamu wote. Kabla ya Ukumbusho, hotuba ya pekee ya watu wote hutolewa ili kuwafanya watu watazamie kwa hamu tukio hilo na kuwachochea wanaopendezwa wajifunze Biblia.
31 Mashahidi wa Yehova hutazamia kwa hamu pindi za kukusanyika pamoja kwenye mikutano, ambako ‘tunafikiriana ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.’ (Ebr. 10:24) Mtumwa mwaminifu na mwenye busara huwa macho ili kupanga mikutano hiyo kulingana na mahitaji yetu ya kiroho. Watumishi wote wa Yehova pamoja na watu wote wanaopendezwa wanahimizwa kuthamini sana mpango wa kukusanyika pamoja kwa ukawaida. Watumishi wa Mungu huunganishwa kwa umoja wanapothamini maandalizi ambayo Yehova anafanya kupitia tengenezo lake. Jambo muhimu zaidi, tunamsifu na kumtukuza Yehova.—Zab. 111:1.
-
-
Wahudumu wa Habari NjemaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 8
Wahudumu wa Habari Njema
YEHOVA alimtuma Mwanaye, Yesu Kristo, ili atuwekee kielelezo bora cha kuiga. (1 Pet. 2:21) Mtu anapokuwa mfuasi wa Yesu, anahubiri habari njema akiwa mhudumu wa Mungu. Akionyesha kwamba jambo hilo lingeburudisha kiroho, Yesu alisema: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha. Chukueni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili yenu.” (Mt. 11:28, 29) Wote ambao wamekubali mwaliko huo wameona ahadi hiyo ikitimia!
2 Akiwa Mhudumu Mkuu wa Mungu, Yesu alichagua watu fulani wawe wafuasi wake. (Mt. 9:9; Yoh. 1:43) Aliwazoeza katika huduma na kuwatuma wafanye kazi ileile aliyokuwa akifanya. (Mt. 10:1–11:1; 20:28; Luka 4:43) Baadaye aliwatuma wengine 70 wakatangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Luka 10:1, 8-11) Yesu alipowatuma wanafunzi wake, aliwaambia hivi: “Yeyote anayewasikiliza ninyi ananisikiliza mimi pia. Na yeyote anayewapuuza ninyi ananipuuza mimi pia. Isitoshe, yeyote anayenipuuza mimi anampuuza pia Yule aliyenituma.” (Luka 10:16) Kwa kusema hivyo, Yesu alikazia jukumu zito alilowapa wanafunzi wake. Walipaswa kumwakilisha Yesu na Mungu Aliye Juu Zaidi! Ndivyo ilivyo leo kwa wale wanaokubali mwaliko huu wa Yesu: Njoo “uwe mfuasi wangu.” (Luka 18:22; 2 Kor. 2:17)
-