-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13 Kuanzia Pentekoste ya 33 W.K. na kuendelea, Mungu alipanda ‘miti mikubwa ya haki’ kama hiyo, yaani Wakristo watiwa-mafuta walio na moyo mkuu. Aliwapanda katika makao ya kiroho ya taifa lake jipya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Baada ya karne nyingi kupita, hatimaye idadi ya “miti” hiyo imekuwa 144,000, na inazaa matunda ya uadilifu ili kumrembesha, au kumtukuza, Yehova Mungu. (Ufunuo 14:3) Wale wa mwisho wa “miti” hiyo yenye fahari wamesitawi katika miaka ya tangu 1919, wakati Yehova alipowahuisha mabaki wa Israeli wa Mungu kutoka kwenye hali yao ya kutotenda kwa muda. Kwa kuwapa maji tele ya kiroho, inaweza kusemwa kwamba Yehova ametokeza msitu wa miti ya haki, yenye kuzaa matunda.—Isaya 27:6.
-