Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Mfereji wa Mawasiliano

      5. Ufunuo uliwasilishwaje kwa mtume Yohana na kisha kwa makundi?

      5 Ufunuo 1:1b, 2, NW unaendelea kusema: “Na yeye [Yesu] alituma malaika wake na kuutoa [Ufunuo] kwa njia ya ishara kupitia yeye kwa mtumwa wake Yohana, ambaye alitoa ushahidi kwa neno ambalo Mungu alitoa na kwa ushahidi ambao Yesu Kristo alitoa, hata kwa mambo yote ambayo yeye aliona.” Hivyo, Yohana alipokea maandishi yaliyovuviwa kupitia mjumbe wa kimalaika. Yeye aliuandika katika hati-kunjo, akiupeleka kwa makundi ya wakati wake. Kwa furaha yetu, Mungu ameuhifadhi kwa ajili ya kitia-moyo cha yale makundi karibu 100,000 ya watumishi wake wenye umoja duniani leo.

      6. Yesu alitambulishaje ule mfereji ambao angetumia kuandalia ‘watumwa’ wake chakula cha kiroho leo?

      6 Mungu alikuwa na mfereji wa kuwasilisha Ufunuo katika siku ya Yohana, na Yohana alikuwa ndiye sehemu ya kidunia ya njia hiyo. Vivyo hivyo, Mungu ana njia ya kutolea ‘watumwa’ wake ulishaji wa kiroho leo. Katika unabii wake mkubwa kuhusu umalizio wa mfumo wa mambo, Yesu alitambulisha sehemu ya njia hii ya kidunia kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu, ambaye, Bwana-mkubwa wake aliweka juu ya watu wake wa nyumba, kuwapa chakula chao kwa wakati unaofaa.” (Mathayo 24:3, 45-47, NW) Yeye anatumia jamii hii ya Yohana katika kufungua maana ya unabii huo.

      7. (a) Ishara zinazopatikana katika Ufunuo zapasa zituathirije sisi? (b) Baadhi ya wale wa jamii ya Yohana wamekuwa wakishiriki katika utimizo wa njozi za Ufunuo kwa muda mrefu kadiri gani?

      7 Mtume Yohana anaandika kwamba Yesu alitoa Ufunuo “kwa njia ya ishara,” au alama. Hiyo iko wazi na inasisimua kuichunguza. Hiyo inaonyesha utendaji wenye msukumo na inapasa, ituchochee, tutie jitihada za bidii katika kujulisha wengine unabii huu na maana yao. Ufunuo unatutolea njozi kadhaa zenye kusisimua, ambazo katika kila mojapo Yohana alishiriki ama kwa kutenda au akiwa mtazamaji. Wale wa jamii ya Yohana, ambao baadhi yao kwa muda unaopita makumi ya miaka wameshiriki katika utimizo wa njozi hizi, wanafurahi kwamba roho ya Mungu imefungua ile maana ili waweze kuifafanua kwa wengine.

  • Vitu Ambavyo Lazima Vitukie Karibuni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 9. (a) Kama Yohana, jamii ya Yohana imeonyesha mwelekeo gani? (b) Yohana anaonyeshaje njia ambayo kwayo sisi tunaweza kuwa wenye furaha?

      9 Yohana alikuwa mwaminifu katika kutoa ushuhuda wa ule ujumbe ambao Mungu alimpa kupitia Yesu Kristo. Yeye alieleza kirefu “vitu vyote ambavyo yeye aliona.” Ile jamii ya Yohana imetafuta kwa hamu nyingi mwongozo kutoka kwa Mungu na Yesu Kristo ili ielewe unabii huo kikamili na kujulisha watu wa Mungu mambo yao mema. Kwa manufaa ya kundi lililopakwa mafuta (na pia ya umati mkubwa wa kimataifa ambao Mungu atahifadhi hai kuipita ile dhiki kubwa), Yohana anaandika hivi: “Mwenye furaha ni yeye ambaye husoma kwa sauti kubwa na wale ambao husikia maneno ya unabii huu, na ambao hushika vitu vilivyoandikwa katika huo; kwa kuwa wakati uliowekwa u karibu.”—Ufunuo 1:3, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki