-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17. (a) Washirika wa Israeli wa Mungu wataitwaje? (b) Ni dhabihu gani moja tu inayohitajiwa ili kuwe na msamaha wa dhambi?
17 Namna gani juu ya Israeli wa Mungu? Yehova anawaambia hivi, kupitia Isaya: “Bali ninyi mtaitwa makuhani wa BWANA; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao.” (Isaya 61:6)
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19. Wakristo watiwa-mafuta watapendelewa kufanya utumishi gani?
19 Zaidi ya hilo, washirika wa Israeli wa Mungu wana tazamio la kutumikia wakiwa makuhani kwa njia nyingine. Wakiisha kufa, wanafufuliwa mbinguni wakiwa roho wasioweza kufa. Licha ya kutumikia wakiwa watawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake huko, wanatumikia pia wakiwa makuhani wa Mungu. (Ufunuo 5:10; 20:6) Katika hali hiyo, watapendelewa kutumia faida za dhabihu ya fidia ya Yesu kuelekea wanadamu waaminifu duniani. Katika njozi ya mtume Yohana iliyoandikwa katika Ufunuo sura ya 22, wanatajwa tena kuwa “miti.” “Miti” yote 144,000 inaonwa ikiwa mbinguni, ikitokeza ‘mazao kumi na mawili ya matunda, ikitoa matunda yake kila mwezi. Na majani ya hiyo miti yalikuwa ya kuponya mataifa.’ (Ufunuo 22:1, 2) Lo, huo ni utumishi wa kikuhani ulio mzuri kama nini!
-