-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na wao wakaja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu moja.” (Ufunuo 20:4c, NW) Je! hii inamaanisha kwamba mahakimu hawa hawafufuliwi mpaka baada ya uharibifu wa mataifa na Shetani na roho waovu wake kutiwa ndani ya abiso? Hapana. Walio wengi wao tayari wako hai sana, kwa kuwa walipanda farasi pamoja na Yesu dhidi ya mataifa kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 2:26, 27; 19:14) Kweli kweli, Paulo alionyesha kwamba ufufuo wao unaanza upesi baada ya kuwapo kwa Yesu kuanza katika 1914 na kwamba baadhi yao hufufuliwa mbele ya wengine. (1 Wakorintho 15:51-54; 1 Wathesalonike 4:15-17) Kwa hiyo, kuja kwao kwenye uhai kunatukia kwa kipindi fulani cha wakati wanapopokea mmoja mmoja zawadi ya uhai usioweza kufa katika mbingu.—2 Wathesalonike 1:7; 2 Petro 3:11-14.
-
-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Ule Ufufuo wa Kwanza
16. Yohana huelezaje habari ya ufufuo wanaoupata wale wanaotawala pamoja na Kristo, na kwa nini?
16 Kurudi sasa kwa wale ambao ‘walikuja kwenye uhai na wakatawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo,’ Yohana aandika: “Huu ndio ufufuo wa kwanza.” (Ufunuo 20:5b) Ni wa kwanza jinsi gani? Ni “ufufuo wa kwanza” kwa habari ya wakati, kwa maana wale wanaoupata ni “matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 14:4, NW) Pia ni wa kwanza kwa umaana, kwa kuwa wale wanaoushiriki wanakuwa watawala wenzi wa Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu na wanahukumu mabaki ya aina ya binadamu. Kwa kumalizia, ni wa kwanza katika ubora. Isipokuwa Yesu Kristo mwenyewe, hao wanaoinuliwa katika ufufuo wa kwanza ndio viumbe pekee wanaosemwa katika Biblia kuwa wanapokea kutokufa.—1 Wakorintho 15:53; 1 Timotheo 6:16.
17. (a) Yohana huelezaje habari ya taraja lenye kubarikiwa la Wakristo wapakwa-mafuta? (b) “Kifo cha pili” ni nini, na kwa nini “hakina mamlaka” juu ya washindi 144,000?
17 Ni taraja lenye baraka kama nini kwa ajili ya hawa wapakwa-mafuta! Kama anavyojulisha wazi Yohana? “Mwenye furaha na mtakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hawa kifo cha pili hakina mamlaka.” (Ufunuo 20:6a, NW) Kama vile Yesu alivyoahidi Wakristo katika Smirna, washindi hawa ambao wanashiriki “ufufuo wa kwanza” hawatakuwa katika hatari ya kupata dhara kutoka “kifo cha pili,” ambacho humaanisha utowesho, uharibifu pasi na tumaini la ufufuo. (Ufunuo 2:11; 20:14, NW) Kifo cha pili “hakina mamlaka” juu ya washindi kama hao, kwa maana wao watakuwa wamekwisha kuvaa kutofisidika na kutokufa.—1 Wakorintho 15:53.
-