-
Msimamizi-nyumba Mwaminifu na Baraza Lake LinaloongozaMnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Mtumwa, au msimamizi-nyumba huyo ni nani, naye anatoa jinsi gani ‘chakula kwa wakati unaofaa’? Ni jambo la maana kwetu sote kutambua njia ambayo inatumiwa kutoa chakula hicho cha kiroho.
3. (a) Wasomi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo wanasema maneno ya Yesu kuhusu yule “mtumwa” yanawahusu nani? (b) Yule “msimamizi-nyumba,” au “mtumwa” ni nani, na “watumishi,” au ‘watumishi wa nyumbani’ ni nani?
3 Mara nyingi wasomi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo wanafikiri kwamba maneno hayo ya Yesu yanawahusu wale ambao wana vyeo vya madaraka kati ya wale wanaodai kuwa Wakristo. Lakini Yesu, ambaye ni “bwana” katika mfano huo, hakusema kwamba kungekuwa na watumwa wengi waliotawanyika katika madhehebu au dini mbalimbali zinazodai kuwa za Kikristo. Badala yake, alisema waziwazi kwamba kungekuwa na “msimamizi-nyumba” au “mtumwa” mmoja tu, ambaye Yesu angemweka juu ya mali zake zote. Kwa hiyo, kama vile ambavyo gazeti hili limeeleza mara nyingi, msimamizi-nyumba huyo anawakilisha “kundi dogo” la wanafunzi watiwa-mafuta wakiwa kikundi. Katika mistari mingine ya Injili ya Luka, Yesu alikuwa amezungumza kuhusu wanafunzi hao. (Luka 12:32) Maneno “watumishi,” au ‘watumishi wa nyumbani’ yanahusu kikundi hichohicho lakini yanakazia daraka lao wakiwa mtu mmoja-mmoja.
-
-
Msimamizi-nyumba Mwaminifu na Baraza Lake LinaloongozaMnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Mtumwa Mwaminifu Katika Siku Zetu
11. Mtumwa aliwekwa rasmi juu ya “mali” gani?
11 Maneno ya Yesu katika Mathayo 24:45 yanaonyesha wazi kwamba bado kungekuwa na jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara duniani katika siku za mwisho. Andiko la Ufunuo 12:17 linawaita watu hao kuwa “waliobaki” wa uzao wa mwanamke. Wakiwa kikundi, mabaki hao wamewekwa rasmi juu ya mali zote za Kristo hapa duniani. “Mali” ambazo msimamizi-nyumba mwaminifu amewekwa rasmi kutunza ni mambo yote ya Bwana huyo yanayohusu Ufalme duniani. Mali hizo zinatia ndani raia wa kidunia wa Ufalme huo na vifaa na majengo yanayotumiwa katika kazi ya kuhubiri habari njema.
-