Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wamehesabiwa Kuwa Wanastahili Kuupokea Ufalme
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Januari 15
    • Uzao wa Abrahamu Unatangazwa Kuwa Mwadilifu

      6, 7. (a) Uzao wa Abrahamu ungekuwa “kama nyota za mbinguni” katika njia gani? (b) Abrahamu alipokea baraka gani, nao uzao wake unapokea baraka gani inayofanana na hiyo?

      6 Abrahamu aliambiwa kwamba uzao wake ungeongezeka na kuwa “kama nyota za mbinguni” na chembe za mchanga zilizo kando ya bahari. (Mwa. 13:16; 22:17) Kwa maneno mengine, katika siku za Abrahamu wanadamu hawangeweza kujua hesabu ya wale ambao wangefanyiza uzao huo. Hata hivyo, mwishowe hesabu kamili ya uzao wake wa kiroho ilifunuliwa. Mbali na Yesu, hesabu yao ingekuwa 144,000.—Ufunuo 7:4; 14:1.

      7 Kuhusu imani ya Abrahamu, Neno la Mungu linasema hivi: “[Abrahamu] akawa na imani katika Yehova; naye akamhesabia kuwa ni uadilifu.” (Mwa. 15:5, 6) Ni kweli kwamba hakuna mwanadamu aliye mwadilifu kabisa. (Yak. 3:2) Hata hivyo, kwa sababu ya imani ya pekee ya Abrahamu, Yehova alishughulika naye kana kwamba alikuwa mwadilifu na hata alimwita rafiki yake. (Isa. 41:8) Wale ambao pamoja na Yesu wanafanyiza uzao wa kiroho wa Abrahamu, wamehesabiwa pia kuwa waadilifu, na hilo linawaletea baraka nyingi zaidi hata kuliko zile alizopokea Abrahamu.

      8. Ni baraka gani zinazotolewa kwa washiriki wa uzao wa Abrahamu?

      8 Wakristo watiwa-mafuta wanahesabiwa kuwa waadilifu kwa sababu wana imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu. (Rom. 3:24, 28) Machoni pa Yehova, wameondolewa hatia ya dhambi na wanaweza kutiwa mafuta kwa roho takatifu na kuwa wana wa kiroho wa Mungu, ndugu za Yesu Kristo. (Yoh. 1:12, 13) Wanaingizwa katika agano jipya na wanafanyiza taifa jipya, “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:16; Luka 22:20) Hilo ni pendeleo kubwa kama nini! Kwa sababu ya mambo yote hayo ambayo Mungu anawatendea, Wakristo watiwa-mafuta hawatumaini kuishi milele duniani. Wanadhabihu tumaini hilo kwa ajili ya shangwe isiyoelezeka ya kushirikiana na Yesu wakati wa Siku ya Hukumu na kutawala pamoja naye huko mbinguni.—Soma Waroma 8:17.

  • Wamehesabiwa Kuwa Wanastahili Kuupokea Ufalme
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Januari 15
    • 12. Paulo aliwakumbusha nini Wakristo watiwa-mafuta?

      12 Wakristo wa karne ya kwanza walitangazwa kuwa waadilifu na kutiwa mafuta kwa roho takatifu ili waweze kupokea urithi wao wa kimbingu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki