Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumia Kila Siku ya Maisha Yako kwa Utukufu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • Wajali Wengine

      Yehova anataka tuwajali wengine na kuwatendea mema. Lakini, Shetani anataka tuwe na ubinafsi. Ulimwengu wake umejaa watu ambao ‘wanajipenda wenyewe’ na “wanaopenda raha” na pia wale ‘wanaopanda kwa mwili wao.’ (2 Tim. 3:1-5; Gal. 6:8) Wengi hawafikirii matokeo ya mambo wanayowatendea wengine. “Matendo ya mwili” yanaonekana kila mahali.—Gal. 5:19-21.

      Wale wanaoongozwa na roho takatifu ya Yehova wako tofauti kabisa, wanaonyesha sifa kama vile upendo, fadhili, na wema wanaposhughulika na wengine. (Gal. 5:22) Neno la Mungu linatuambia tutangulize kwanza mahitaji ya wengine. Hivyo, tunapendezwa kikweli na wengine, ingawa tunakuwa waangalifu kwamba tusiingilie mambo yao ya kibinafsi. (1 Kor. 10:24, 33; Flp. 2:3, 4; 1 Pet. 4:15) Tunawaonyesha ufikirio zaidi waamini wenzetu. Hata hivyo, tunajitahidi pia kuwasaidia wale ambao si waamini. (Gal. 6:10) Je, unaweza kutafuta fursa ya kumtendea kwa fadhili mtu fulani leo?—Ona sanduku “Wajali Wengine,” kwenye ukurasa wa 23.

      Hatupaswi kuwajali wengine pindi fulani au katika hali fulani tu. (Gal. 6:2; Efe. 5:2; 1 The. 4:9, 10) Badala yake, kila siku tunajitahidi kutambua uhitaji wa wengine na kuwa tayari kuwasaidia, hata inapokuwa vigumu kufanya hivyo. Tunataka kuwaonyesha wengine ukarimu kwa chochote tulicho nacho iwe ni wakati wetu, vitu vyetu vya kimwili, uzoefu, au hekima yetu. Yehova anatuhakikishia kwamba tukiwaonyesha wengine ukarimu, atatuonyesha ukarimu pia.—Met. 11:25; Luka 6:38.

  • Tumia Kila Siku ya Maisha Yako kwa Utukufu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 23]

      Wajali Wengine

      • Ndugu au dada mzee.—Law. 19:32.

      • Mtu mgonjwa au mwenye matatizo ya kihisia.—Met. 14:21.

      • Mshiriki wa kutaniko mwenye uhitaji ambao unaweza kutimiza.—Rom. 12:13.

      • Mshiriki wa karibu wa familia yako.—1 Tim. 5:4, 8.

      • Mwamini mwenzetu ambaye amefiwa na mwenzi wa ndoa.—1 Tim. 5:9.

      • Mzee wa kutaniko lenu mwenye bidii.—1 The. 5:12, 13; 1 Tim. 5:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki