Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • 21. (a) Kile kipindi cha wakati kilichotabiriwa katika Danieli 12:11 kingeanza wakati ambapo hali gani zingetokea? (b) Ile “sadaka ya kuteketezwa daima” ilikuwa nini, nayo iliondolewa lini? (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 298.)

      21 Danieli aliambiwa hivi: “Tangu wakati ule ambapo sadaka ya kuteketezwa ya daima itaondolewa, na hilo chukizo la uharibifu litakaposimamishwa, itapata siku elfu na mia mbili na tisini.” Kwa hiyo, kipindi hicho cha wakati kingeanza wakati ambapo hali fulani zingekuwa zimetokezwa. “Sadaka ya kuteketezwa ya daima”a ilikuwa imeondolewa. (Danieli 12:11) Malaika huyo alimaanisha dhabihu gani? Si dhabihu ya wanyama iliyotolewa kwenye hekalu lolote la kidunia. Kwani, hata hekalu ambalo wakati mmoja lilikuwa Yerusalemu lilikuwa “nakala ya uhalisi”—hekalu kuu la kiroho la Yehova, lililoanza kutumika wakati Kristo alipopata kuwa Kuhani wa Cheo cha Juu wa hekalu hilo mwaka wa 29 W.K.! Katika hekalu hilo la kiroho, lenye kuwakilisha mpango wa Mungu wa ibada safi, hakuna uhitaji wa matoleo yenye kuendelea ya dhambi, kwa kuwa ‘Kristo alitolewa mara moja kwa wakati wote ili kuchukua dhambi za wengi.” (Waebrania 9:24-28) Hata hivyo, Wakristo wote wa kweli hutoa dhabihu kwenye hekalu hilo. Mtume Paulo aliandika hivi: “Kupitia [Kristo] acheni sikuzote tumtolee Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo ambayo hulifanyia jina lake tangazo la hadharani.” (Waebrania 13:15) Kwa hiyo, hali hiyo ya kwanza ya unabii huo—kule kuondolewa kwa “sadaka ya kuteketezwa daima”—ilitimizwa katikati ya mwaka wa 1918 wakati ambapo kazi ya kuhubiri ilionekana kana kwamba ilikuwa imekomeshwa kwa muda.

  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • KUONDOLEWA KWA SADAKA YA KUTEKETEZWA DAIMA

      Katika kitabu cha Danieli, maneno “sadaka ya kuteketezwa daima” (au “sadaka ya kuteketezwa kila siku”) yapatikana mara tano. Yarejezea dhabihu ya sifa—“tunda la midomo”—ambayo watumishi wa Yehova Mungu humtolea kwa ukawaida. (Waebrania 13:15) Kuondolewa kwake kulikotabiriwa kwarejezewa kwenye Danieli 8:11, 11:31, na 12:11.

      Wakati wa vita viwili vya ulimwengu, watu wa Yehova walinyanyaswa vikali katika milki za “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini.” (Danieli 11:14, 15) “Sadaka ya kuteketezwa daima” iliondolewa kuelekea mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, wakati ambapo kazi ya kuhubiri ilikaribia sana kusimamishwa kwa muda katikati ya mwaka wa 1918. (Danieli 12:7)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki