-
Kutegemeza Kazi ya Ufalme Kwenu na Ulimwenguni PoteTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
KUGAWA MACHAPISHO
16 Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia husaidia sana kueneza ujumbe wa Ufalme. Kwa kawaida baraza la wazee humpa mtumishi wa huduma mgawo wa kutunza machapisho ya kutaniko. Ndugu waliopewa migawo hiyo huchukua majukumu yao kwa uzito. Wanaweka rekodi nzuri ya machapisho ili kutosheleza mahitaji ya kutaniko.
17 Tukiwa Wakristo waliojiweka wakfu, tunatambua kwamba wakati wetu, akili na nguvu, vipaji, mali zetu, hata uhai wetu wenyewe ni zawadi kutoka kwa Mungu na tunapaswa kuzitumia katika utumishi wake. (Luka 17:10; 1 Kor. 4:7) Tunapotumia vizuri kila kitu tulicho nacho, tunaonyesha kwamba tunampenda sana Yehova. Tunatamani sana kumheshimu Yehova kwa vitu vyetu vyenye thamani, tukijua kwamba anapendezwa na zawadi yoyote tunayomtolea ili kuonyesha kwamba tumejitoa kwake kwa nafsi yote. (Met. 3:9; Marko 14:3-9; Luka 21:1-4; Kol. 3:23, 24) Yesu alisema: “Mlipokea bure, toeni bure.” (Mt. 10:8) Tunapojitoa wenyewe na kila kitu tulicho nacho katika utumishi wa Yehova, tunapata shangwe kubwa sana.—Mdo. 20:35.
-
-
“Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 13
“Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”
TUKIWA watumishi wa Mungu waliojiweka wakfu, tuna wajibu wa kusema na kufanya mambo yote kwa utukufu wa Yehova. Mtume Paulo alitoa kanuni inayotuongoza alipoandika hivi: “Iwe mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Hilo linatia ndani kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Yehova vinavyoonyesha utu wake mkamilifu. (Kol. 3:10) Ni lazima tumwige Mungu tukiwa watu watakatifu.—Efe. 5:1, 2.
2 Akikazia umuhimu wa Wakristo kuwa watakatifu, mtume Petro aliandika hivi: “Kama watoto watiifu, acheni kufinyangwa na tamaa mlizokuwa nazo zamani katika hali yenu ya kutojua, lakini iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote kama Yule Mtakatifu aliyewaita ninyi, kwa maana imeandikwa: ‘Lazima muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.’” (1 Pet. 1:14-16) Kama Waisraeli wa kale, wote katika kutaniko la Kikristo wanapaswa kudumisha utakatifu. Hilo linamaanisha kwamba wanapaswa kubaki safi na kuepuka kuchafuliwa na dhambi na mambo yasiyofaa ya ulimwengu. Hivyo wanatakaswa kwa ajili ya utumishi wa Yehova.—Kut. 20:5.
3 Utakatifu unadumishwa kwa kufuata sheria na kanuni za Yehova zinazotajwa waziwazi katika Maandiko
-