Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Toleo la Hiari ili Kuendeleza Ibada Safi
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Hata hivyo, kazi hiyo ya ujenzi haingehitaji michango na vifaa tu. Yehova pia aliwaambia Waisraeli hivi: “Kila mtu kati yenu aliye na moyo wa hekima na aje, na kuyafanya hayo yote ambayo BWANA ameyaagiza.” Naam, kazi hiyo ya ujenzi ilihitaji wafanyakazi wenye ustadi. Kwa kweli, “kazi za werevu kila aina”—kutia ndani useremala, uhunzi, na upambaji kwa vito—zingehitajiwa ili kukamilisha kazi hiyo. Bila shaka, Yehova angeelekeza vipawa vya wafanyakazi hao, na kwa kufaa yeye angepata sifa ambayo ingetokana na kufanikiwa kwa kazi hiyo.—Kutoka 35:10, 30-35; 36:1, 2.

  • Toleo la Hiari ili Kuendeleza Ibada Safi
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Katika hali nyinginezo, ndugu na dada Wakristo hutumia ustadi mwingi walio nao kusaidia kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na majengo ya ofisi za tawi. Kisha kuna kazi ambayo hufanywa katika makao ya Betheli zaidi ya mia moja ulimwenguni kote, ambayo yahusisha ustadi mwingi tofauti-tofauti. Wote wenye moyo wa kupenda ambao wametoa michango hiyo wanaweza kuwa na hakika kwamba Yehova hatasahau kazi yao ngumu!—Waebrania 6:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki