“Kuongozwa na Roho ya Mungu”
Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova
◼ MAELFU ya makusanyiko hayo ya siku tatu, yaliyoanza nchini Marekani Mei 23-25, yatafanywa miezi ijayo katika maelfu ya majiji ulimwenguni pote. Mnamo 2007, watu zaidi ya milioni 12 walihudhuria makusanyiko zaidi ya 3,200 kama hayo!
Katika maeneo mengi mwaka huu, kila siku programu itaanza saa 3:20 asubuhi kwa kipindi cha muziki. Kichwa cha programu ya Ijumaa (Siku ya 5), kinachotegemea Yohana 16:13, ni “Roho . . . Atawaongoza Ninyi Ndani ya Kweli Yote.” “Kwa Nini Tuongozwe na Roho ya Mungu?” na “Roho Takatifu Katika Uumbaji!” zitakuwa miongoni mwa hotuba za kwanza. Mfululizo “Waaminifu wa Kale—Waliongozwa na Roho ya Mungu” utakuwa na sehemu hizi, “Nyakati za Musa,” “Nyakati za Waamuzi,” na “Karne ya Kwanza.” Hotuba ya msingi, “Fungu la Roho Takatifu Katika Kutimizwa kwa Kusudi la Yehova,” itamalizia kipindi cha asubuhi.
Ijumaa alasiri, sehemu ya kwanza itakuwa “Majibu ya Maswali Kuhusu Roho Takatifu,” nayo itafuatwa na hotuba, “Roho Huchunguza Ndani ya . . . Mambo Mazito ya Mungu” na “Iweni Wasikiaji na Watendaji wa Neno la Mungu.” Mfululizo wenye kichwa “Vijana—Tembeeni kwa Roho Takatifu!” utakuwa na sehemu hizi, “Shuleni,” “Kazini,” “Katika Familia,” “Kutanikoni,” “Nyakati za Burudani,” na “Unapokuwa Peke Yako.” Jambo kuu la kusanyiko siku hiyo litakuwa hotuba ya mwisho yenye kichwa “Vijana—Lindeni Uhusiano Wenu na Yehova,” nayo itawasaidia kufanya hivyo.
Kichwa cha programu ya Jumamosi ni ‘Kupanda kwa Roho,’ kinachotegemea Wagalatia 6:8. Kipindi cha asubuhi kitatia ndani mfululizo wa sehemu tatu wenye kichwa “Kuongozwa na Roho ya Mungu Katika Huduma.” Kipindi hicho kitamalizika baada ya hotuba ya ubatizo kisha wale wanaostahili watabatizwa.
Hotuba ya kwanza Jumamosi alasiri, “Waandikaji wa Biblia—‘Waliongozwa na Roho Takatifu,’” itafuatwa na mfululizo wenye sehemu tano ulio na kichwa “Tumewezeshwa na Roho Takatifu” “Kupinga Majaribu,” “Kukabiliana na Uchovu na Kuvunjika Moyo,” “Kuvumilia Mateso,” “Kutofuata Umati,” na “Kuvumilia Shida.” Jambo lingine kuu la kusanyiko litakuwa hotuba ya mwisho ya siku hiyo yenye kichwa “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu.”
Programu ya Jumapili itakuwa na kichwa “Endeleeni Kutembea kwa Roho,” kinachotegemea Wagalatia 5:16. Mfululizo wenye sehemu tisa “Sitawisha ‘Matunda ya Roho’” utazungumzia kila sehemu ya matunda ya roho yaliyotajwa katika Wagalatia 5:22, 23. Hotuba ya watu wote “Pata Baraka Kupitia Mfalme Anayeongozwa na Roho!” itamalizia kipindi cha asubuhi. Sehemu ya pekee ya kipindi cha alasiri ni drama yenye waigizaji “Usiache ‘Upendo Uliokuwa Nao Mwanzoni.’” Inaonyesha mitazamo na hali ambazo huenda zilikuwako miongoni mwa Wakristo mwishoni mwa karne ya kwanza. Kusanyiko litamalizika kwa hotuba “Kutumikia kwa Uaminifu na Tengenezo la Yehova Linaloongozwa na Roho.”
Fanya mipango sasa ili uhudhurie. Ili kujua kusanyiko lililo karibu nawe litafanyika wapi, tembelea Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova au waandikie wachapishaji wa gazeti hili. Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 2008 (1/3/2008), lina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Rwanda, Tanzania, na Uganda.