Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kabla ya Mashahidi wa Yehova kukutana katika Madison Square Garden jijini New York mwaka 1939, matisho yalitolewa na wafuasi wa padri Mkatoliki Charles Coughlin kwamba kusanyiko hilo lingevunjwa. Polisi walijulishwa. Mnamo Juni 25, Ndugu Rutherford alisema kwa watu 18,000 au zaidi waliokuwa katika jumba hilo, kutia na wasikilizaji wengi wa kimataifa kwa njia ya redio, juu ya kichwa “Serikali na Amani.” Baada ya hotuba hiyo kuanza, Wakatoliki wa Roma na Wanazi 200 au zaidi, wakiongozwa na mapadri kadhaa Wakatoliki, walisongamana kwenye roshani. Baada ya kutolewa kwa ishara fulani, walianza kuvuma kwa sauti, wakipiga kelele kusema “Heil Hitler!” na “Viva Franco!” Walitumia kila aina ya lugha chafu na vitisho na kuwapiga wakaribishaji wengi waliochukua hatua kuzima mchafuko huo. Magenge hayo hayakufanikiwa kuvunja mkutano huo. Ndugu Rutherford aliendelea kusema kwa nguvu na bila kuogopa. Kwenye kilele cha mvurugo huo, alijulisha hivi: “Angalieni leo Wanazi na Wakatoliki ambao wangependa kuvunja mkutano huu, lakini kwa neema ya Mungu hawawezi kufanya hivyo.” Wasikilizaji waliunga mkono hilo kwa makofi mazito ya kurudiarudia. Mchafuko huo ulinaswa na vinasasauti katika pindi hiyo, na umesikiwa na watu katika sehemu nyingi za ulimwengu.

  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 657]

      Wakati kusanyiko hili la Mashahidi lilipofanywa katika New York mwaka 1939, wanagenge kama 200 wakiongozwa na mapadri Wakatoliki walijaribu kulivunja

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki