-
Kukusanyika Ili Tumsifu YehovaHuduma ya Ufalme—2003 | Juni
-
-
5 Sikiliza na Ujifunze: Ezra aliutayarisha moyo wake kwa sala ili kupokea neno la Mungu. (Ezra 7:10) Aliuelekeza moyo wake ili kupokea mafundisho ya Yehova. (Mit. 2:2) Tunaweza kuanza kutayarisha mioyo yetu kwa ajili ya kusanyiko hata kabla ya kuondoka nyumbani kwa kutafakari kichwa cha kusanyiko na kukizungumzia na familia yetu.
6 Kwenye ukumbi mkubwa au uwanja wa kusanyiko kwaweza kuwa na vikengeusha-fikira vingi. Vikengeusha-fikira hivyo vyaweza kugeuza fikira zetu kutoka kwa msemaji, na kutufanya tukose habari muhimu. Madokezo yaliyo kwenye sanduku lililoonyeshwa hapa yanaweza kutusaidia tuboreshe uwezo wetu wa kukaza fikira.
-
-
Kukusanyika Ili Tumsifu YehovaHuduma ya Ufalme—2003 | Juni
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 3]
Kusikiliza Kwenye Kusanyiko
▪ Tafakari vichwa vya hotuba
▪ Fungua maandiko
▪ Andika maandishi machache
▪ Andika mambo makuu ya kutumia
▪ Rudia mambo unayojifunza
-