-
Kutumia Maswali VizuriFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Ili Kuendeleza Mazungumzo. Unapokuwa katika utumishi wa shambani, uwe macho kuona pindi za kuwaomba watu maoni yao ikiwa hawaoni ubaya kuulizwa maswali.
Mashahidi wengi huanzisha mazungumzo yenye kupendeza kwa kuuliza swali kama, “Je, umewahi kufikiria . . . ?” Wakichagua swali ambalo watu wengi wanalifikiria sana, hakika watafurahia utumishi wa shambani. Hata kama mtu hajawahi kusikia swali ambalo umeuliza, bado linaweza kuchochea fikira zake. Tunaweza kuzungumzia mambo mengi kwa kuuliza maswali kama “Unaonaje . . . ?” na “Je, unaamini . . . ?”
Mweneza-evanjeli Filipo alimwendea ofisa wa makao ya kifalme kutoka Ethiopia ambaye alikuwa akisoma kwa sauti unabii wa Isaya. Filipo akamwuliza: “Je, wewe kwa hakika wajua [au, unaelewa] unayoyasoma?” (Mdo. 8:30) Swali hilo lilimwezesha Filipo amweleze kweli kuhusu Yesu Kristo. Mashahidi wengine leo wametumia swali kama hilo kuzungumza na watu ambao wametamani sana kuelewa vizuri kweli ya Biblia.
Watu wengi husikiliza wakipewa nafasi ya kutoa maoni. Baada ya kuuliza swali, sikiliza kwa makini. Uwe mwenye fadhili badala ya kuchambua jibu la mtu huyo. Mpongeze kutoka moyoni inapowezekana. Pindi moja, Yesu alimpongeza mwandishi mmoja ambaye ‘alijibu kwa kutumia akili,’ akamwambia: ‘Hauko mbali na ufalme wa Mungu.’ (Mk. 12:34) Hata kama hukubaliani naye, unaweza kumshukuru kwa kujieleza. Maneno yake yanaweza kukuonyesha mambo unayohitaji kufikiria unapozungumza naye kweli ya Biblia.
-