Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Anataka Watu Wapate Uzima—Je, Ndivyo Unavyotaka Pia?
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • 14, 15. Mtazamo wetu kuhusu msamaha wa Yehova unaweza kujaribiwa katika hali gani?

      14 Namna gani ikiwa ndugu aliyetenda dhambi nzito alikosa kutubu na ikabidi atengwe na ushirika wa kutaniko? Ndivyo ilivyotukia katika karne ya kwanza. Wakristo ambao walitenda dhambi na kukosa kutubu walitengwa na ushirika. Ikiwa jambo hilo lilitukia mitume wa Yesu wakiwapo, haishangazi kwamba linatukia mara kwa mara leo. Katika visa hivyo, washiriki washikamanifu kutanikoni hukubali mwongozo wa Biblia wa kutoshirikiana na mtu aliyetengwa na ushirika. Ushikamanifu wao kwa Yehova unaweza kumsaidia mkosaji huyo kuona ubaya wa mwenendo wake usiofaa, na hilo laweza kumsukuma atubu. Tunasoma katika Biblia kwamba mtu fulani huko Korintho aliyetengwa na ushirika, alirudishwa kutanikoni baada ya kutubu na kugeuka. (1 Wakorintho 5:11-13; 2 Wakorintho 2:5-8) Mtu anaporudishwa leo, wewe huhisije, na utaonyeshaje kwamba ungependa wengine pia wapate uzima?

  • Yehova Anataka Watu Wapate Uzima—Je, Ndivyo Unavyotaka Pia?
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • Kuhusu yule Mkorintho aliyerudishwa ambaye ametajwa awali, Paulo aliwahimiza washiriki wa kutaniko wamsamehe na kumtia moyo, na kumhakikishia kwamba walimpenda kikweli: “Kemeo hili linalotolewa na walio wengi linamtosha mtu wa namna hiyo, . . . mnapaswa kumsamehe kwa fadhili na kumfariji, ili kwa njia fulani mtu huyo asimezwe na huzuni yake ya kupita kiasi. Kwa hiyo nawahimiza ninyi kumthibitishia upendo wenu.” (2 Wakorintho 2:6-8)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki