Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Wakorintho
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • MTUME Paulo anahangaikia sana hali ya kiroho ya kutaniko la Korintho. Amesikia kwamba kuna migawanyiko kati ya ndugu huko. Upotovu wa maadili unaachiliwa. Pia, kutaniko limemwandikia Paulo ili kuomba mwongozo kuhusu mambo fulani. Hivyo, yapata mwaka wa 55 W.K., Paulo anapokuwa Efeso wakati wa safari yake ya tatu ya umishonari, anaandika barua yake ya kwanza kati ya barua zake mbili kwa Wakorintho.

  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Wakorintho
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • ‘KAENI MACHO, SIMAMENI IMARA, IWENI NA NGUVU’

      (1 Kor. 1:1–16:24)

      Paulo anahimiza hivi: “Nyote mseme kwa upatano.” (1 Kor. 1:10) ‘Hakuna msingi mwingine wowote kuliko Yesu Kristo,’ ambao juu yake sifa za Kikristo zinajengwa. (1 Kor. 3:11-13) Kuhusu mwasherati katika kutaniko, Paulo anasema hivi: “Ondoeni yule mtu mwovu kati yenu.” (1 Kor. 5:13) “Mwili si kwa ajili ya uasherati,” anasema, “bali kwa ajili ya Bwana.”—1 Kor. 6:13.

      Ili kujibu “mambo ambayo [waliandika],” Paulo anatoa mashauri mazuri kuhusu ndoa na useja. (1 Kor. 7:1) Baada ya kueleza kuhusu ukichwa wa Kikristo, utaratibu kwenye mikutano ya Kikristo, na uhakikisho wa ufufuo, Paulo anatoa himizo hili: “Kaeni macho, simameni imara katika imani, endeleeni kuwa kama wanaume, iweni na nguvu.”—1 Kor. 16:13.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      1:21—Je, ni kweli kwamba Yehova anatumia “upumbavu” ili kuwaokoa waamini? Hapana, hafanyi hivyo. Hata hivyo, kwa kuwa “ulimwengu kupitia hekima yake haukuja kumjua Mungu,” njia anazotumia ili kuwaokoa watu zinaonekana kuwa upumbavu kwa ulimwengu.—Yoh. 17:25.

      5:5—Ni nini maana ya maneno, “mkamkabidhi mtu [mwovu] kwa Shetani kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili, ili roho iokolewe”? Mtu anayezoea kutenda dhambi nzito bila kutubu anapotengwa na kutaniko, anakuwa tena sehemu ya ulimwengu mwovu wa Shetani. (1 Yoh. 5:19) Hivyo, inasemwa kuwa amekabidhiwa kwa Shetani. Kutengwa kwa mtu huyo kunaharibu au kunaondoa uvutano mbaya wa mtu huyo katika kutaniko na kunalinda roho au mtazamo wa kutaniko.—2 Tim. 4:22.

      7:33, 34—Ni nini maana ya “mambo ya ulimwengu” ambayo mwanamume au mwanamke anayefunga ndoa anahangaikia? Paulo anazungumza kuhusu mambo ya maisha ya kila siku ambayo Wakristo waliofunga ndoa wanahitaji kuhangaikia. Mambo hayo yanatia ndani chakula, mavazi, na makao, lakini hayahusishi mambo mabaya ya ulimwengu ambayo Wakristo wanakataa.—1 Yoh. 2:15-17.

      11:26—Ni kwa njia gani kifo cha Yesu kinapaswa kuadhimishwa “kila mara,” nacho kinapaswa kuadhimishwa “mpaka” wakati gani? Paulo hakuwa akisema kwamba kifo cha Yesu kingeadhimishwa mara nyingi. Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kuwa “kila mara” linamaanisha “wakati wowote ambapo” au “kila wakati ambapo.” Hivyo, Paulo alikuwa akisema kwamba kila mara Wakristo watiwa-mafuta wanapokula mkate na kunywa divai ya Ukumbusho, mara moja kwa mwaka siku ya Nisani 14, ‘wanatangaza kifo cha Bwana.’ Wanafanya hivyo “mpaka atakapofika,” yaani, mpaka atakapowapokea mbinguni kupitia ufufuo.—1 The. 4:14-17.

      13:13—Ni katika njia gani upendo ni mkuu kuliko imani na tumaini? Wakati “mambo yanayotumainiwa” yanapotimia na “tarajio lililohakikishwa” la mambo hayo linapotimizwa, imani na tumaini zinafikia mwisho wake. (Ebr. 11:1) Upendo ni mkuu kuliko imani na tumaini katika maana ya kwamba upendo unadumu milele.

      15:29—Inamaanisha nini ‘kubatizwa kwa kusudi la kuwa wafu’? Paulo hakuwa akipendekeza kwamba watu walio hai wabatizwe kwa ajili ya wale waliokufa bila kubatizwa. Hapa Paulo anazungumza kuhusu kubatizwa kwa Wakristo watiwa-mafuta katika maisha yanayohusisha kushika utimilifu mpaka wanapokufa na kufufuliwa kwenye uhai wa roho.

      Mambo Tunayojifunza:

      1:26-31; 3:3-9; 4:7. Kujisifu katika Yehova kwa unyenyekevu, badala ya kujisifu wenyewe, kunadumisha umoja katika kutaniko.

      2:3-5. Alipokuwa akihubiri huko Korintho, kituo cha elimu na falsafa ya Kigiriki, huenda Paulo alihangaikia ikiwa angeweza kuwashawishi wasikilizaji wake. Hata hivyo, hakuruhusu udhaifu wowote au woga ambao huenda alikuwa nao umzuie asitimize huduma aliyopewa na Mungu. Vivyo hivyo, hatupaswi kuruhusu hali zisizo za kawaida zituzuie tusitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu. Kama Paulo, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atatusaidia.

      2:16. Kuwa na “akili ya Kristo” ni kujua njia yake ya kufikiri, kufikiri kama anavyofikiri, kuelewa kabisa utu wake, na kuiga kielelezo chake. (1 Pet. 2:21; 4:1) Ni jambo la maana kama nini kujifunza kwa uangalifu maisha na huduma ya Yesu!

      3:10-15; 4:17. Tunapaswa kuchunguza na kuboresha uwezo wetu wa kufundisha na kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Ikiwa hatufundishi vizuri, huenda wanafunzi wetu wakashindwa na majaribu ya imani, na huenda tukapata hasara kubwa hivi kwamba tutaokolewa “kama kupitia katika moto.”

      6:18. ‘Kukimbia uasherati’ si kuepuka tu matendo ya por·neiʹa bali pia ponografia (picha au habari za ngono), uchafu wa kiadili, mawazo mapotovu, kuwachezea wengine kimapenzi—jambo lolote ambalo linaweza kuongoza kwenye uasherati.—Mt. 5:28; Yak. 3:17.

      7:29. Wenzi wa ndoa wanapaswa kuwa waangalifu ili wasihangaikiane sana na hivyo kukosa kutanguliza mambo ya Ufalme.

      10:8-11. Yehova alikasirika sana Waisraeli walipomnung’unikia Musa na Haruni. Ni jambo la hekima kuepuka kusitawisha zoea la kunung’unika.

      16:2. Tutatoa michango ya pesa kwa ukawaida ili kuendeleza kazi ya Ufalme ikiwa tutafanya mipango mapema na kutoa michango hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki