-
Wewe Hutoaje Shauri?Mnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
3 Tumia Neno la Mungu kwa Unyenyekevu.
“Sifanyi jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe; bali kama vile Baba alivyonifundisha, ndivyo ninavyosema mambo haya.”—YOH. 8:28.
Je, utasema, “Kama ningekuwa wewe, ninge . . .”? Hata kama jibu la swali uliloulizwa linaonekana kuwa wazi, itakuwa vizuri kwako kujifunza kutokana na mfano wa unyenyekevu na kiasi ambao Yesu alituwekea. Alikuwa na uzoefu na hekima nyingi zaidi kuliko mwanadamu yeyote; hata hivyo, alisema hivi: “Sijasema kutokana na msukumo wangu mwenyewe, bali Baba mwenyewe . . . amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.” (Yoh. 12:49, 50) Sikuzote mafundisho na mashauri ya Yesu yalitegemea mapenzi ya Baba yake.
Kwa mfano, katika Luka 22:49 tunasoma kwamba Yesu alipokuwa karibu kukamatwa wanafunzi wake walimuuliza ikiwa walipaswa kupigana. Mwanafunzi mmoja alitumia upanga. Angalia simulizi linalofanana na hilo katika Mathayo 26:52-54 linaonyesha kwamba hata chini ya hali hizo, Yesu alitumia wakati wake kumsaidia mwanafunzi huyo kuelewa mapenzi ya Yehova. Akitambua kanuni iliyo katika Mwanzo 9:6 na unabii wa Zaburi 22 na Isaya 53, Yesu aliweza kutoa mwongozo wenye hekima ambao bila shaka uliokoa uhai wa watu na kumpendeza Yehova.
-
-
Wewe Hutoaje Shauri?Mnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 9]
Kwa sababu ya maandalizi ambayo Yehova anatupatia kupitia tengenezo lake, tunaweza kutoa na kupokea mashauri yaliyo bora kabisa. Andiko la Mhubiri 12:11 linasema hivi: “Maneno ya wenye hekima ni kama michokoo ya kuongoza ng’ombe, na kama tu misumari iliyopigiliwa ndani, ndivyo walivyo wale wanaoshughulika mno kukusanya maneno; wametolewa kutoka kwa mchungaji mmoja.” Kama tu “michokoo ya kuongoza ng’ombe,” yaani, vijiti vilivyochongoka vinavyotumiwa kuongoza wanyama wavutao mizigo, ndivyo mashauri mazuri na yenye upendo yanavyowaongoza watu wanyoofu upande unaofaa. “Misumari iliyopigiliwa ndani” inafanya majengo yawe imara. Vivyo hivyo, kutoa mashauri mazuri kunaweza kuwaimarisha wengine. Watu wenye hekima ‘wanashughulika mno,’ au wanafurahia sana ‘kukusanya maneno’ ambayo yanategemea hekima ya ‘mchungaji wao mmoja,’ Yehova.
Mwige Mchungaji huyo unapotoa shauri. Ni pendeleo kubwa kama nini kwetu kusikiliza kwa makini na pia kutoa shauri lenye faida inapowezekana! Shauri letu linapotegemea kikweli kanuni za Biblia, litakuwa zuri na linaweza kumnufaisha milele msikilizaji.
-