Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Iweni Hodari na Wenye Moyo wa Ushujaa!’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Machi 1
    • Vielelezo vya Ujasiri Tunavyopaswa Kuiga

      12. Yesu aliweka kielelezo gani bora cha kuwa jasiri, naye aliwatiaje moyo wafuasi wake?

      12 Tunaweza kupata msaada wa kusitawisha ujasiri tukizingatia vielelezo vya wengine ambao wametenda kwa ujasiri kama Yeremia. (Zaburi 77:12) Kwa mfano, tunapochunguza huduma ya Yesu, tunavutiwa na ujasiri alioonyesha aliposhawishiwa na Shetani na alipopingwa vikali na viongozi Wayahudi. (Luka 4:1-13; 20:19-47) Kwa nguvu za Yehova, Yesu alikuwa thabiti sana, na muda mfupi kabla ya kifo chake aliwaambia wanafunzi wake: “Ulimwenguni mnakuwa na dhiki, lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.” (Yohana 16:33; 17:16) Ikiwa wanafunzi wa Yesu wangefuata kielelezo chake, wao pia wangeshinda. (1 Yohana 2:6; Ufunuo 2:7, 11, 17, 26) Lakini wangehitaji ‘kujipa moyo.’

      13. Paulo aliwapa Wafilipi kitia-moyo gani?

      13 Miaka kadhaa baada ya kifo cha Yesu, Paulo na Sila walifungwa gerezani katika jiji la Filipi. Baadaye, Paulo alitia moyo kutaniko la Filipi liendelee ‘kusimama imara katika roho moja, kwa nafsi moja likipigana sambamba kwa ajili ya imani ya habari njema, na bila kuogopeshwa sana katika jambo lolote na wapinzani wao.’ Ili kuwatia moyo waendelee kusimama imara, Paulo alisema: “Jambo hilihili [kuteswa kwa Wakristo] ni ithibati kwao ya uangamizo [kwa wanaowatesa], lakini ya wokovu kwenu; na wonyesho huu ni kutoka kwa Mungu, kwa sababu nyinyi mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si kuweka tu imani yenu katika yeye, bali pia kuteseka kwa ajili yake.”—Wafilipi 1:27-29.

      14. Ujasiri wa Paulo huko Roma ulikuwa na matokeo gani?

      14 Paulo alipoandikia kutaniko la Filipi, alikuwa gerezani tena, wakati huo alikuwa amefungwa huko Roma. Hata hivyo, aliendelea kuwahubiria wengine kwa ujasiri. Matokeo yakawaje? Aliandika: “Vifungo vyangu vimejulikana kwa watu wote kwa kushirikiana na Kristo miongoni mwa Walindaji wa Praetori wote na wale wengine wote; na walio wengi zaidi kati ya akina ndugu katika Bwana, wakihisi uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, wanaonyesha moyo mkuu hata zaidi kulisema neno la Mungu bila hofu.”—Wafilipi 1:13, 14.

  • ‘Iweni Hodari na Wenye Moyo wa Ushujaa!’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Machi 1
    • Wakristo wa mapema walisitawishaje ujasiri? Fikiria kilichotukia wakati makuhani wakuu na wazee huko Yerusalemu walipowaambia Petro na Yohana wakome kuhubiri katika jina la Yesu. Wanafunzi hao walikataa, wakatishwa, kisha wakaachiliwa. Mara tu baada ya hapo, walijiunga tena na ndugu zao, na wote wakasali pamoja wakisema: “Yehova, yaangalie matisho yao, na kuwaruhusu watumwa wako kufuliza kusema neno lako kwa ujasiri wote.” (Matendo 4:13-29) Yehova alijibu sala yao kwa kuwaimarisha kwa roho takatifu, na kama viongozi Wayahudi walivyosema baadaye, ‘wakajaza Yerusalemu’ kwa mafundisho yao.—Matendo 5:28.

      9 Na tuchunguze mambo yaliyotokea wakati huo. Wanafunzi walipotishwa na viongozi Wayahudi, hawakuacha kuhubiri kwa sababu ya mateso. Badala yake, wanafunzi hao waliomba wapewe ujasiri ili waendelee kuhubiri. Kisha wakatenda kulingana na sala yao, naye Yehova akawaimarisha kwa roho yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki