-
Malezi ya Mtoto—Maoni YaliyosawazikaAmkeni!—1997 | Desemba 8
-
-
Malezi ya Pamoja
Mahakimu wengine huhisi kwamba ni muhimu kusitawisha uwasiliano kati ya mtoto na wazazi wote wawili. Kusababu kwao kwategemezwa na chunguzi za utafiti zinazoonyesha kwamba watoto wanaweza kupatwa na mkazo na madhara ya kihisia-moyo kidogo zaidi baada ya talaka ikiwa wazazi wataweza kushiriki malezi. Badala ya kuhisi kuwa ametupwa na mzazi mmoja, mtoto huyo atakuwa na hisi ya kupendwa na wazazi wote wawili na kushirikishwa katika nyumba zote mbili. “Malezi ya pamoja ni njia ya kuwahusisha wazazi wote wawili,” asema mwanasheria mmoja wa familia.
-
-
Malezi ya Mtoto—Maoni YaliyosawazikaAmkeni!—1997 | Desemba 8
-
-
Malezi ya Mzazi Mmoja
Huenda mahakama ikampa malezi mzazi ambaye, katika maoni yake, aweza kuandaa vizuri zaidi mahitaji ya mtoto. Huenda hakimu akaamua kwamba mzazi mlezi awe ndiye pekee afanyaye maamuzi kwa habari ya masuala ya maana yanayohusu hali njema ya mtoto. Mara nyingi, mahakama hufikia uamuzi huo baada ya kusikiliza matokeo ya uchunguzi wa wakadiriaji—hawa kwa kawaida huwa ni wanasaikolojia, madaktari wa magonjwa ya akili, au wafanyakazi wa umma.
Watetezi wa malezi ya mzazi mmoja huhisi kuwa mpango huo humwezesha mtoto kuwa imara zaidi. Wazazi wanaposhindwa kuwasiliana au wanapoelekea kutowasiliana pamoja kwa matokeo, mahakimu wengi wa kesi hupendelea mpango huu wa malezi. Bila shaka, mzazi asiye mlezi haachwi nje kabisa ya maisha ya mtoto. Haki za kutumia wakati pamoja na mtoto kwa kawaida hupewa mzazi asiye mlezi, na wazazi wote wawili wanaweza kuendelea kumwandalia mtoto mwongozo, upendo, na shauku inayohitajiwa.
-