Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 5/15 uku. 32
  • ‘Washukuruni Mashahidi wa Yehova kwa Uhuru wa Kidini’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Washukuruni Mashahidi wa Yehova kwa Uhuru wa Kidini’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 5/15 uku. 32

‘Washukuruni Mashahidi wa Yehova kwa Uhuru wa Kidini’

“KABLA ya kukataa kuzungumza na Shahidi wa Yehova, tua na ufikirie ule mnyanyaso wenye kufedhehesha ambao walivumilia majuzi tu. Na fikiria jinsi walivyosaidia kuimarisha haki za Marekebisho ya Kwanza (ya katiba ya Marekani), ambazo hutunufaisha sisi sote,” yasema makala moja ya gazeti la USA Today. Mashahidi wa Yehova walinyanyaswa Marekani katika miaka ya 1940, kwa sababu walikataa kusalimu bendera na kwa sababu ya masuala mengine.—Kutoka 20:4, 5.

Kesi 30 hivi ambazo zilihusu Mashahidi wa Yehova zilipelekwa Mahakama Kuu ya Marekani katika kipindi cha miaka mitano, kutoka mwaka wa 1938 hadi 1943. Makala hiyo yasema: “Mashahidi walipeleka mahakamani masuala yaliyohusu mambo ya msingi ya Marekebisho ya Kwanza mara nyingi hivi kwamba Hakimu Harlan Fiske Stone aliandika hivi: ‘Mashahidi wa Yehova wapaswa kulipwa kwa sababu wamesaidia kutatua matatizo mengi ya kisheria kuhusiana na haki mbalimbali za raia.’”

Kisha, makala hiyo yamalizia kwa kusema: “Dini zote zapasa kuwashukuru Mashahidi wa Yehova kwa kuwa waliimarisha uhuru wa [kidini] kwa njia nyingi sana.”

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Jengo linaloonekana nyuma: Photo by Josh Mathes, Collection of the Supreme Court of the United States; chini kushoto, mahakimu: Collection of the Supreme Court of the United States

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki