Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kusudi la Yehova Lafanikiwa
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
    • 9. Andiko la Waroma 8:21 linawaahidi nini wanadamu?

      9 Watu hao wenye tumaini la kuishi duniani wanasubiri kwa hamu wakati ambapo wanadamu wote ‘watawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu.’ (Waroma 8:21) Wataanza kuwekwa huru baada ya Kristo na majeshi yake ya mbinguni kukomesha dhiki kubwa wakati wa Har–Magedoni. Ulimwengu wote mwovu wa Shetani utaharibiwa wakati huo, halafu Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja utaleta baraka.—Ufunuo 19:17-21; 20:6.

  • Kusudi la Yehova Lafanikiwa
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
    • Uhuru Mzuri Ajabu Utakaokuwapo Wakati Ujao

      11. Waokokaji wa dhiki kubwa watafurahia uhuru gani wa ajabu?

      11 Dhiki kubwa iishapo wakati wa Har–Magedoni, uovu utakuwa umekomeshwa duniani, na Shetani Ibilisi hatakuwa tena “mungu wa huu mfumo wa mambo.” Waabudu wa Yehova hawatapambana tena na uvutano mwovu wa Shetani. (2 Wakorintho 4:4; Ufunuo 20:1, 2) Dini isiyo ya kweli haitamletea Yehova suto tena wala kuwagawanya wanadamu. Watumishi wa Mungu wa kweli hawatadhulumiwa wala kuteswa tena na mamlaka za wanadamu. Watafurahia uhuru mzuri ajabu!

      12. Wanadamu wote watawekwaje huru kutoka katika dhambi na madhara yake?

      12 Yesu, yule “Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi ya ulimwengu,” atafuta dhambi zote za wanadamu akitumia thamani ya dhabihu yake. (Yohana 1:29) Yesu alipokuwa duniani, aliwaponya watu kwa kuwasamehe dhambi zao. (Mathayo 9:1-7; 15:30, 31) Vivyo hivyo, Kristo Yesu, akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu huko mbinguni, atawaponya kimuujiza vipofu, mabubu, viziwi, walemavu, wenye ugonjwa wa akili, na wale wenye magonjwa mengine yoyote. (Ufunuo 21:3, 4) “Sheria ya dhambi” ambayo watu wote watiifu wanayo itafutiliwa mbali hivi kwamba mawazo na matendo yao yatakuwa yenye kupendeza kwao wenyewe na kwa Mungu. (Waroma 7:21-23) Mwishoni mwa Miaka Elfu Moja, wanadamu watakuwa wakamilifu, katika ‘sura na mfano’ wa Mungu wa pekee wa kweli.—Mwanzo 1:26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki