Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nilipata Majaribu Makali Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Katika mji jirani wa Sitía, kikundi cha Mashahidi wenye bidii kilianzishwa. Jambo hili lilimwudhi askofu wa hapo. Yeye alikuwa ameishi Marekani na alijua kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa na matokeo sana katika kazi yao ya kuhubiri. Hivyo akaazimia kumaliza “uasi-imani” huo katika eneo lake. Mara kwa mara aliwachochea polisi kuwakamata Mashahidi na kuwafunga gerezani na kuwapeleka mahakamani kwa mashtaka mbalimbali ya uwongo.

  • Nilipata Majaribu Makali Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Mnamo Februari 1945 ndugu yangu Demosthenes aliyesadiki kwamba Mashahidi wa Yehova wanafundisha kweli, alinipa kijitabu Comfort All That Mourn (Faraja kwa Wote Wanaoomboleza).d Nilivutiwa na kijitabu hicho. Tuliacha kwenda Kanisa Othodoksi mara moja, tukajiunga na kikundi kile kidogo huko Sitía, na kuwahubiria ndugu na dada zetu juu ya imani yetu mpya. Wote walikubali kweli ya Biblia. Kama nilivyotarajia, uamuzi wangu wa kuacha dini ya uwongo ulileta uhasama kutoka kwa mke wangu na familia yao, nao wakanitenga. Baba mkwe wangu alikataa kuongea nami kwa muda fulani. Kulikuwa na ugomvi na mgogoro sikuzote nyumbani. Hata hivyo, Mei 21, 1945, mimi na Demosthenes tulibatizwa na Ndugu Minos Kokkinakis.e

      Mwishowe niliweza kutimiza mradi wa maisha yangu na kutumikia kama mhudumu wa kweli wa Mungu! Bado nakumbuka siku yangu ya kwanza katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Nilisafiri peke yangu hadi kijiji fulani nikiwa na vijitabu 35 mkobani. Nilianza kwenda nyumba kwa nyumba kwa woga. Lakini kadiri nilivyosonga mbele ndivyo nilivyopata ujasiri zaidi. Wakati kasisi mmoja mwenye hasira kali alipowasili, nilisimama imara kwa ujasiri, na kukataa kwenda naye kwenye kituo cha polisi, ijapokuwa alisisitiza niende. Nilimwambia kwamba singeondoka kabla ya kumaliza kuwahubiria watu wote kijijini humo, na ndivyo nilivyofanya. Nilikuwa na furaha nyingi hivi kwamba hata sikungojea basi bali nilitembea kwa miguu hadi nyumbani, umbali wa kilometa 15.

      Mkononi mwa Majambazi Wakatili

      Mnamo Septemba 1945, nilikabidhiwa madaraka zaidi katika kutaniko letu jipya huko Sitía.

  • Nilipata Majaribu Makali Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Kisha, mwaka wa 1986, niliombwa niende kusaidia kutaniko la Sitía, Krete. Nilifurahi kukubali kwenda kutumikia tena katika kutaniko nilipoanza utumishi langu wa Kikristo, na kutumikia pamoja na waamini wenzangu wapendwa ambao nimewajua tangu ujana wangu.

  • Nilipata Majaribu Makali Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • [Picha katika ukurasa wa 29]

      Nikihubiri pamoja na Shahidi mwenzangu huko Sitía, Krete, nilikotumikia nikiwa kijana

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki