Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Tatizo la Uhalifu Linaweza Kutatuliwa?
    Amkeni!—2008 | Februari
    • Dakt. Stanton E. Samenow anaandika hivi kuhusu njia za sasa za kukabiliana na uhalifu: “Baada ya kufungwa gerezani, [mhalifu] anaweza kujifunza mbinu za kuwa mjanja na mwangalifu zaidi, lakini anaendelea na njia yake ya maisha na kuzidi kufanya uhalifu. Takwimu zinazoonyesha ikiwa mtu amerudia kufanya uhalifu huonekana tu mtu anapokamatwa tena.” Kwa hiyo, magereza yamekuwa kama vyuo vya wahalifu, yakiwasaidia bila kukusudia kuboresha ustadi wao.—Ona sanduku “Je, Magereza Ni Vyuo vya Uhalifu?” kwenye ukurasa wa 7.

      Isitoshe, mara nyingi wahalifu hawaadhibiwi, na hivyo kuwafanya wafikiri kwamba uhalifu una faida. Maoni hayo yanawafanya wawe jasiri na sugu zaidi. Mtawala mmoja mwenye hekima alisema hivi: “Kwa maana hukumu juu ya kazi mbaya haikutekelezwa upesi, ndiyo sababu moyo wa wana wa binadamu umeazimia kabisa ndani yao kutenda yaliyo mabaya.”—Mhubiri 8:11.

  • Je, Tatizo la Uhalifu Linaweza Kutatuliwa?
    Amkeni!—2008 | Februari
    • Uhalifu Huanzia Moyoni

      Biblia inakazia mtu wa ndani na si hali zake. Yakobo 1:14, 15 inasema: “Kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi.” Mtu anapofikiria mawazo mabaya, anakuza tamaa mbaya. Hilo linaweza kumwongoza atende mabaya. Kwa mfano, kupendezwa kijuu-juu tu na picha au habari za ngono kunaweza kumwongoza mtu apendezwe kupita kiasi na ngono, na hilo linaweza kumsukuma atende kulingana na tamaa zake, labda hata kwa kuvunja sheria.

      Jambo lingine tunalopaswa kutilia maanani ni kwamba ulimwengu hukazia ubinafsi, pesa, raha, na kutosheleza tamaa mara moja. Biblia ilitabiri hivi kuhusu nyakati zetu: “Katika siku za mwisho . . . , watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, . . . wakali, wasiopenda wema, [na] wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu.” (2 Timotheo 3:1-5) Inasikitisha kwamba kupitia sinema, michezo ya video, vitabu na watu mashuhuri ambao hawaweki mfano mzuri, ulimwengu huendeleza tabia ambazo huchochea uhalifu zaidi.b

  • Je, Tatizo la Uhalifu Linaweza Kutatuliwa?
    Amkeni!—2008 | Februari
    • a Ugonjwa wa akili unaweza kuchangia uhalifu, hasa kwenye nchi ambazo wagonjwa hao wanaachwa waranderande mitaani ambako wanaweza kupata silaha. Hata hivyo, makala hii haizungumzii suala hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki