-
Je, Wajua?Amkeni!—2004 | Aprili 8
-
-
Majibu ya Maswali
1. Mahali pa familia pa kuzikia
2. Umande na manyoya ya kondoo
3. “Vazi rasmi kutoka Shinari” pamoja na fedha na dhahabu
4. “Mwili mmoja”
5. Uaguzi, uchawi, kutafuta ishara za bahati, ulozi, kufunga wengine kwa kuwatakia maovu, kutafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo, kubashiri matukio, na kadhalika
6. Alifanya karamu kubwa, akatoa msamaha kwa wilaya zake za utawala, na kutoa zawadi
7. ‘Watachukiwa’
8. Kozbi, binti ya Suri
9. “Mke mwenye uwezo”
10. Mwana wa tatu wa Daudi, Absalomu
11. Alipinga jinsi Daudi alivyokuwa “akiruka na kucheza dansi huku na huku mbele za Yehova” kwa shangwe
12. “Vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote”
13. Wayahudi kutoka Antiokia na Ikoniamu walifika, wakaushawishi umati ufanye hivyo
14. Aliuchomoa upanga wake na kumpiga yule mtumwa aliyeitwa Malko, akalikata sikio lake la kuume
15. Amfanyie “tendo la ibada”
16. Chachu
17. Ethani, Hemani, Kalkoli, na Darda
-
-
Usichelewe!Amkeni!—2004 | Aprili 8
-
-
sababu ya hekima na utukufu.” (Mhubiri 10:1) Naam, “upumbavu kidogo” tu kwa kukosa kuwafikiria wengine, unaweza kukuharibia sifa mbele ya mwalimu au mwajiri.
Alipokuwa akisomea kwenye chuo kimoja, mwanamke anayeitwa Marie alitambua kwamba baadhi ya wanafunzi wenzake “hawakujali wakati,” kwani mara nyingi walikuwa wakichelewa. “Hata hivyo iliwabidi wabadilike,” anakumbuka. “Profesa wawili walizingatia sana wakati. Kwa hiyo wanafunzi walipochelewa dakika chache, walihesabiwa kuwa hawakufika. Na baada ya kutofika mara kadhaa mwanafunzi alianguka mtihani.”
Tatizo la kuchelewa linaweza kukuharibia sifa zako mbele ya marafiki. Mwanamume wa makamo anayeitwa Joseph anamkumbuka Mkristo mwenzake aliyemjua miaka mingi iliyopita. Ijapokuwa mwanamume huyo aliheshimiwa kwa sababu ya uwezo wake wa kufundisha, alikuwa na tatizo lenye kuaibisha. “Alikuwa akichelewa sikuzote,” akumbuka Joseph. “Alikuwa akichelewa kwa kila kitu! Naye hakujali hata kidogo. Watu walimtania kuhusu kuchelewa kwake.” Je, watu wameanza kukutaja kuwa mtu ambaye huchelewa kila wakati? Ikiwa ndivyo, huenda basi wasione sifa zako nzuri.
● WAFIKIRIE WENGINE. Kuchelewa ni kukosa adabu na huwakengeusha wengine. Na kunaweza kufanya watu wafikiri kwamba unajiona kuwa bora sana. Akieleza sababu zinazowafanya wasimamizi wa makampuni kuchelewa kufika mikutanoni, mfanyabiashara mmoja alikiri hivi: “Wengi wetu wana kiburi.” Tofauti na hilo, Wakristo huwaona wengine kuwa bora kuliko wao wenyewe. (Wafilipi 2:3) Wao pia hutumia ile kanuni ya kuwatendea wengine kama wanavyotaka kutendewa. (Mathayo 7:12) Je, wewe huudhika unapolazimika kuwangojea wengine? Basi usiwafanye wengine wakungojee.
● JIFUNZE JINSI YA KUTUMIA WAKATI. Je, wewe huahirisha mambo na kuharakisha dakika za mwisho-mwisho? Je, wewe hujipangia mambo mengi kupita kiasi, na kujaribu kuyafanya kwa wakati mfupi sana? Kanuni ya Mhubiri 3:1 inaweza kukusaidia: “Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu.” Ukiwa na “wakati uliowekwa” kwa ajili ya mambo utayafanya kwa utaratibu.
-