-
Je, Wajua?Amkeni!—2003 | Juni 8
-
-
Majibu kwa Maswali
1. Mwanamke Mfilisti wa Timna
2. Mali
3. Boazi
4. Yahweh
5. ‘Mbwa wangemla Yezebeli’
6. Ili amzike Sara mke wake humo
7. “Jifunge viuno”
8. Sethi
9. Akani
10. “Jozi moja ya njiwa-tetere au hua wachanga wawili”
11. Kama mtume wa Kristo Yesu
12. Kwa sababu Senakeribu alijisifu kwa kusema kwamba Yehova hana uwezo, kama ile miungu ya mataifa yaliyokuwa yameshindwa
13. Huko Troasi, bandari iliyoko Asia Ndogo
14. Kwa kuwa wakati huo Mfalme Asa alikuwa ameungana na mfalme wa Siria badala ya kumtegemea Yehova kwa sababu isiyojulikana
15. “Hadi mwisho”
-
-
Epuka Usemi UnaoumizaAmkeni!—2003 | Juni 8
-
-
Vivyo hivyo, Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Usichambue mwanamume mzee kwa ukali.” (1 Timotheo 5:1) Kanuni hiyo inaweza kutumiwa tunaposhughulika na watu wote. Biblia inatutia moyo ‘tusiseme kwa ubaya juu ya yeyote, tusiwe wataka-vita, tuwe wenye kukubali sababu, tukionyesha wazi upole wote kuelekea watu wote.’—Tito 3:2.
Kuzuia Midomo Yetu
Wakati mwingine, si rahisi kuepuka kishawishi cha kuwashambulia wengine kwa maneno. Mtu akikosewa, anaweza kuhisi akiwa na haki ya kumwadhibu yule aliyemkosea kwa maneno makali, yenye kuumiza, iwe ni kwa kusema naye au kwa kumsengenya. Lakini, Wakristo hukinza mwelekeo huo. Andiko la Mithali 10:19 husema hivi: “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.”
Malaika wa Mungu huweka mfano mzuri. Wao wanajua makosa yote ambayo wanadamu hufanya. Ingawa malaika wana uwezo na nguvu nyingi kuliko wanadamu, hawawashtaki wanadamu kwa matusi, “kwa sababu ya kumstahi Yehova.” (2 Petro 2:11) Kwa kuwa wanajua Mungu anajua makosa ya kila mtu na anaweza kurekebisha mambo, malaika huizuia midomo yao. Mikaeli, yule malaika mkuu, hakuthubutu kutumia matusi, hata dhidi ya Ibilisi.—Yuda 9.
Wakristo hujitahidi kuwaiga malaika. Wanafuata himizo hili la Biblia: “Msirudishe ovu kwa ovu kwa yeyote. Andaeni mambo bora mbele ya macho ya watu wote. Ikiwezekana, kwa kadiri itegemeavyo nyinyi, iweni wenye kufanya amani na watu wote. Wapendwa, msijilipizie kisasi wenyewe bali iachieni nafasi hasira ya kisasi; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; hakika mimi nitalipa, asema Yehova.’”—Waroma 12:17-19.
Hata hali na kiasi cha sauti yetu kinaweza kuumiza. Waume na wake huumizana mara nyingi kwa kufokeana kwa sauti ya juu. Wazazi wengi huwafokea watoto wao. Hata hivyo, haifai kupiga makelele tunapoelezea hisia zetu. Biblia inatusihi hivi: “Acheni uchungu wote wenye nia ya kudhuru na hasira na hasira ya kisasi na kupiga kelele na usemi wenye kuudhi viondolewe mbali kutoka kwenu.” (Waefeso 4:31) Pia Biblia inasema kwamba “mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali ahitaji kuwa mwanana kuelekea wote.”—2 Timotheo 2:24.
Maneno Yanayoponya
Kwa kuwa usemi wenye kuumiza na mizaha imeenea sana leo, Wakristo wanapaswa kutafuta njia ya kujizuia wasiyatumie. Biblia inasema njia nzuri ni kumpenda jirani. (Mathayo 7:12; Luka 10:27) Tukiwajali na kuwapenda majirani, hiyo itatusaidia kutumia maneno yanayoponya kila siku. Biblia inasema hivi: “Msiache usemi uliooza utoke kinywani mwenu, bali usemi wowote ule ulio mwema kwa ajili ya kujenga kama vile kuwezavyo kuwa na uhitaji, ili huo upate kuwapa wasikiaji lililo la kupendeleka.”—Waefeso 4:29.
Pia, Neno la Mungu likipenya akilini mwetu, litatusaidia kuepuka usemi wenye kuumiza. Kusoma na kutafakari Maandiko Matakatifu kunaweza kutusaidia ‘kuweka mbali uchafuko wote.’ (Yakobo 1:21) Naam, Neno la Mungu linaweza kuponya akili zetu.
-