-
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na hakutakuwa tena na laana yoyote. Bali kiti cha ufalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo vitakuwa ndani ya jiji, na watumwa wake watatolea yeye utumishi mtakatifu;
-
-
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wakati ukuhani wa Kiisraeli ulipopata kuwa mfisadi, ulipatwa na laana ya Yehova. (Malaki 2:2) “Nyumba” isiyo na imani ya Yerusalemu ilitamkwa na Yesu imeachwa. (Mathayo 23:37-39) Lakini katika Yerusalemu Jipya, “hakutakuwa tena na laana yoyote.” (Linga Zekaria 14:11.) Wakaaji walo wote wamekwisha tahiniwa katika moto wa majaribu hapa duniani, na wakiwa wamekwisha pata ushindi, watakuwa ‘wamekwisha vaa kutofisidika na kutokufa.’ Kwa habari yao, Yehova anajua, kama vile alivyojua kwa habari ya Yesu, kwamba hawataangukia mbali kamwe. (1 Wakorintho 15:53, 57)
-