-
Mazishi ya Kikristo Ni Yenye Heshima, Kiasi, na Yanampendeza MunguMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 15
-
-
Katika Afrika na kwingineko, watu wengi wanaamini kwamba desturi fulani zisipofuatwa, roho za mababu zitakasirika. Kukosa kufuata desturi hizo kunaonwa kuwa kosa zito linaloweza kumfanya mtu alaaniwe na watu katika jamii au apatwe na msiba. Kwa sababu ya kukataa kushiriki katika desturi za mazishi zisizopatana na Maandiko, watu wengi wa Yehova wameshutumiwa, wametukanwa, na kukataliwa na watu wa kijiji chao au watu wa familia zao. Hata wengine wamelaumiwa kuwa watu wasiotaka kuchangamana na wengine na wasiowaheshimu wafu. Nyakati nyingine, watu ambao si waamini wameingilia mipango ya mazishi ya Mkristo.
-
-
Mazishi ya Kikristo Ni Yenye Heshima, Kiasi, na Yanampendeza MunguMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 15
-
-
Katika sehemu nyingi za Afrika, watu wengi wanaamini kwamba ni lazima mazishi yawe na watu wengi na yavutie sana ili roho za mababu zisikasirike. Wengine wanatumia mazishi ‘kuonyesha’ kiwango chao cha maisha na cha kifedha. (1 Yoh. 2:16) Wakati, jitihada, na pesa nyingi zinatumiwa ili aliyekufa apate mazishi “yanayofaa.” Ili kuwavutia watu wengi iwezekanavyo, picha kubwa zenye matangazo kuhusu mtu aliyekufa zinawekwa sehemu mbalimbali, na hivyo watu wote wanatangaziwa kuhusu mazishi. Fulana zenye picha ya aliyekufa zinashonwa na kugawanywa ili waombolezaji wazivae. Sanduku la bei ghali na lenye madoido mengi linanunuliwa ili kuwavutia watazamaji. Katika nchi moja ya Afrika, wengine wanatengeneza masanduku yanayofanana na magari, ndege, mashua, na vitu vingine vinavyoonyesha utajiri, cheo, na anasa. Mwili unaweza kutolewa ndani ya sanduku na kuwekwa juu ya kitanda kilichopambwa kwa njia ya pekee. Mwanamke anaweza kuvalishwa nguo nyeupe ya arusi na kupambwa kwa vito vingi, shanga, na kupodolewa.
-