-
Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za MazishiMnara wa Mlinzi—1998 | Julai 15
-
-
Sherehe za Makesha
Katika nchi nyingi, waombolezaji hukusanyika nyumbani mwa aliyekufa na kukesha usiku kucha. Mara nyingi makesha hayo hutia ndani karamu na muziki wenye sauti ya juu. Inaaminiwa kwamba jambo hilo hutuliza wafu na kulinda familia iliyoachwa dhidi ya uchawi. Huenda hotuba zenye kurai-rai zikatolewa ili kupata upendeleo wa aliyekufa. Baada ya hotuba, huenda waombolezaji wakaimba wimbo wa kidini kabla ya mtu mwingine kusimama na kuzungumza. Huenda wakafanya hivyo hadi mapambazuko.b
Mkristo wa kweli hawezi kushiriki katika sherehe hizo za makesha za usiku kucha kwa sababu Biblia huonyesha kwamba wafu hawawezi kuwasaidia au kuwadhuru walio hai. (Mwanzo 3:19; Zaburi 146:3, 4; Yohana 11:11-14) Maandiko hulaumu zoea la uwasiliani-roho. (Ufunuo 9:21; 22:15) Hata hivyo, huenda mjane Mkristo akashindwa kuwazuia wengine wasianzishe mazoea ya uwasiliani-roho. Huenda wakasisitiza wakeshe usiku kucha nyumbani mwake. Ni nini ambacho waamini wenzi wanaweza kufanya ili kuwasaidia Wakristo waliofiwa ambao wanakabili mnyanyaso huo wa ziada?
Mara nyingi wazee wa kutaniko wameweza kuitegemeza familia ya Kikristo iliyofiwa kwa kusababu na watu wa jamaa na majirani. Baada ya kusababu kama huko, huenda watu hao wakakubali kuondoka nyumbani humo kwa amani na kukusanyika tena siku nyingine kwa ajili ya mazishi. Lakini vipi ikiwa baadhi yao wanakuwa wenye ugomvi? Huenda kuendelea kusababu nao kukatokeza jeuri. ‘Mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali ni lazima afulize kujizuia mwenyewe chini ya uovu.’ (2 Timotheo 2:24) Kwa hiyo, iwapo watu wa jamaa wasiotaka kushirikiana wataka kuongoza mambo kwa nguvu, huenda mjane Mkristo na watoto wake wasiweze kuwazuia. Lakini hawatashiriki katika sherehe ya kidini ya uwongo inayofanywa nyumbani mwao, kwa kuwa wao hutii amri hii ya Biblia: “Msiwe wenye kufungwa nira isiyosawazika pamoja na wasio waamini.”—2 Wakorintho 6:14.
-
-
Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za MazishiMnara wa Mlinzi—1998 | Julai 15
-
-
b Katika vikundi fulani vya lugha na utamaduni, neno “makesha” hutumiwa kumaanisha ziara fupi ya kumfariji aliyefiwa. Huenda ziara hiyo isihusishe jambo lolote lisilo la Kimaandiko. Ona gazeti la Amkeni! la Mei 22, 1979, ukurasa wa 27-28 (la Kiingereza).
-
-
Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za MazishiMnara wa Mlinzi—1998 | Julai 15
-
-
Epuka Kuiga Desturi Zisizo za Kikristo
Watu wengine walio na ujuzi wa Biblia wameogopa kuonekana kuwa tofauti. Ili kuepuka mnyanyaso, wamejaribu kuwapendeza majirani wao kwa kujifanya waonekane kana kwamba wanashika desturi ya makesha kwa ajili ya wafu. Ingawa kuwatembelea waliofiwa ili kuwafariji kibinafsi kwastahili pongezi, jambo hilo halihitaji kwamba kufanywe ibada ndogo ya mazishi kila usiku nyumbani mwa aliyekufa kabla ya mazishi halisi. Huenda kufanya hivyo kukawakwaza watazamaji, kwa kuwa huenda jambo hilo likafanya wafikiri kwamba wanaoshiriki hawaamini kabisa yale Biblia isemayo juu ya hali ya wafu.—1 Wakorintho 10:32.
Biblia huwahimiza Wakristo watangulize ibada ya Mungu maishani na kutumia wakati wao kwa hekima. (Mathayo 6:33; Waefeso 5:15, 16) Ingawa hivyo, katika sehemu fulani, utendaji wa kutaniko umesimamishwa kwa juma moja au hata majuma mengi kwa sababu ya mazishi. Tatizo hilo haliko Afrika pekee. Ripoti kutoka Amerika ya Kusini yasema hivi kuhusiana na mazishi fulani: “Mikutano mitatu ya Kikristo ilikuwa na wahudhuriaji wachache mno. Utumishi wa shambani ukapuuzwa kwa muda wa siku kumi. Hata watu wasio Mashahidi na wanafunzi wa Biblia walishangaa na kukatishwa tamaa kuona baadhi ya ndugu na dada zetu wakishiriki katika shughuli hizo za mazishi.”
-