-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
MAKUSANYIKO YASIYOSAHAULIKA
Mnamo Julai 1955, John Cutforth, mmishonari Mkanada aliyekuwa akitumika huko Australia, aliwasili Port Moresby na kuwa mwangalizi wa kwanza wa mzunguko. Mara moja, John alipenda eneo hilo, utamaduni, na watu wake. Hakujua kwamba angetumika nchini Papua New Guinea kwa zaidi ya miaka 35.
John alifika akiwa na sinema inayoitwa The New World Society in Action, masimulizi yaliyoonyesha utaratibu wa tengenezo na makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova. Wakati wa ziara yake ya majuma matatu, alionyesha sinema hiyo mara 14 nyakati nyingine mbele ya mamia ya wahudhuriaji au hata mbele ya watu 2,000 hivi. Watu wengi sana waliifurahia, hiyo ikiwa mara ya kwanza kwa wengine wao kutazama sinema yoyote.
Ziara ya John ilifikia mwisho wakati wa kusanyiko la mzunguko la siku moja huko Haima. “Wanaotaka kubatizwa walipoombwa wasimame, . . . watu 70 walisimama!” anakumbuka Tom Kitto. “Mioyo yetu ilijawa na shangwe tulipoona ndugu 40 na dada 30 wakisimama msituni kwenye ukingo wa mto wakiwa tayari kuonyesha wakfu wao kwa Yehova.”
-
-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUTUMIA PICHA KUHUBIRI
Mnamo 1957, John Cutforth alihamia kabisa Papua New Guinea na kuwa mwangalizi anayesafiri huko. Tangu ziara yake ya kwanza, alikuwa amefikiria sana njia bora zaidi ya kuwahubiria wenyeji, kwa kuwa wengi wao hawakujua kusoma na kuandika. Sasa alikuwa tayari kutumia mbinu yake.
Alipokuwa akitoa hotuba mbele ya kutaniko au kikundi cha mbali, John aliandika jina lake na la mtafsiri kwenye ubao mweusi. Kisha, akaelekeza kidole mbinguni, na kuwauliza wasikilizaji, “Mungu, jina lake nani?” Akaandika jibu lao, “Yehova” na “Zaburi 83:18” juu ya ubao huo. Chini yake upande wa kushoto, aliandika kichwa “Ulimwengu wa Kale” na kuchora wanaume wawili wakipigana, mtu akilia, kaburi, na “Waroma 5:12.” Upande wa kulia, akaandika kichwa “Ulimwengu Mpya” na kuchora wanaume wawili wakisalimiana kwa mikono, mtu akitabasamu, kaburi lililofutwa, na “Ufunuo 21:4.” Baadaye, alitoa hotuba yenye kusisimua ili kueleza michoro yake. Kisha akawakaribisha wasikilizaji wasimame mbele na kurudia hotuba yake. Walipokuwa wameelewa, aliwaambia wachore picha hizo kwenye karatasi na kuzitumia katika kazi ya kuhubiri.
-
-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 90]
Kulia: John Cutforth akifundisha kwa kutumia picha; chini: ndugu akibeba ubao wenye picha ili akahubiri katika vijiji vya mbali
-