-
“Meli za Kitimu” Zatawala BahariniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
Wakaaji wa Saiprasi na Bahari
Ushuhuda wa vitu vya kale vilivyochimbuliwa baharini na makaburini, na pia maandishi ya kale na michoro kwenye vyombo vya udongo unatusaidia kuwazia jinsi meli za Saiprasi zilivyokuwa. Wakaaji wa kale wa Saiprasi walikuwa watengenezaji stadi wa meli. Kisiwa chao kilikuwa na misitu mikubwa, na ghuba zake zenye kingo zilikuwa bandari za kiasili. Miti haikukatwa tu ili kutengeneza meli bali pia kuyeyusha shaba nyekundu, ambayo ilikuwa mali ya asili iliyofanya Saiprasi iwe mashuhuri katika ulimwengu huo wa kale.
Biashara kubwa ya Saiprasi iliwavutia Wafoinike, ambao walianzisha koloni katika maeneo mbalimbali waliyopitia walipokuwa wakifanya biashara. Jiji la Kition huko Saiprasi lilikuwa moja ya makoloni hayo.—Isaya 23:10-12.
Baada ya Tiro kuanguka, ni wazi kwamba baadhi ya wakaaji wake walikimbilia Kitimu. Inaelekea kwamba wakoloni Wafoinike waliokuwa na uzoefu wa kusafiri baharini walichangia sana teknolojia ya jeshi la baharini la Wasaiprasi. Kition lilikuwa mahali pazuri sana na hivyo liliandaa ulinzi kwa meli za Wafoinike.
Chahusika Katika Biashara Kubwa ya Kimataifa
Shughuli za kale za kibiashara za mashariki ya Mediterania katika kipindi hicho zilikuwa nyingi. Bidhaa za thamani kutoka Saiprasi zilisafirishwa kwa meli hadi Krete, Sardinia, na Sisili na pia katika visiwa vya Aegea. Magudulia na vyombo vya maua kutoka Saiprasi vimepatikana katika maeneo hayo, na vyombo bora vya udongo kutoka Ugiriki vimepatikana kwa wingi huko Saiprasi. Wasomi fulani ambao wamechunguza vipande vya shaba nyekundu vilivyopatikana huko Sardinia, wanaamini kwamba vilitoka Saiprasi.
Mnamo 1982 meli iliyovunjika mwishoni mwa karne ya 14 K.W.K. ilipatikana karibu na pwani ya kusini ya Uturuki. Vitu vingi vyenye thamani vilipatikana chini ya maji. Vitu hivyo vinatia ndani vipande vya shaba nyekundu vinavyoaminika kuwa vilitoka Saiprasi, kaharabu, magudulia ya Wakanaani, mbao za mpingo, pembe za tembo, vito vingi vya Wakanaani vya dhahabu na fedha, na mapambo fulani mfano wa mbawakavu ambaye Wamisri walimwona kuwa mtakatifu, na pia vitu vingine kutoka Misri. Baada ya kuchunguza udongo uliopatikana katika meli hiyo, wachunguzi fulani wamesema kwamba inaelekea meli hiyo ilitoka Saiprasi.
Inapendeza kwamba meli hiyo inakadiriwa kuwa ilivunjika katika kipindi ambacho Balaamu alizungumzia meli za Kitimu kwenye “neno lake la kimethali.” (Hesabu 24:15, 24) Kwa wazi, meli za Saiprasi zilikuwa maarufu sana katika Mashariki ya Kati. Meli hizo zilitengenezwa namna gani?
Meli za Biashara
Maumbo mengi ya udongo ya meli na mashua yamepatikana katika maeneo ya makaburi ya jiji la kale la Amathus huko Saiprasi. Maumbo hayo yanasaidia sana kufahamu aina mbalimbali za meli za Wasaiprasi. Baadhi ya maumbo hayo ya meli yamewekwa katika majumba ya ukumbusho.
Maumbo hayo ya udongo yanaonyesha kwamba kwa wazi meli za mapema zilitumiwa kwa shughuli zenye amani za biashara. Meli ndogo ziliendeshwa na wanaume 20 ambao walipiga makasia. Meli kubwa zilitengenezwa ili kusafirisha bidhaa na abiria ambao walitaka kwenda kwenye maeneo ya karibu kandokando ya pwani ya Saiprasi. Plini Mkubwa anasema kwamba Wasaiprasi waliunda meli nyepesi ambayo iliendeshwa kwa makasia ambayo ingeweza kubeba uzito wa tani 90.
Halafu kulikuwa na meli kubwa za biashara kama ile iliyopatikana karibu na pwani ya Uturuki. Baadhi ya meli hizo zingeweza kubeba mizigo yenye uzito wa tani 450. Idadi ya waliopiga makasia katika meli kubwa ingefikia wanaume 50, wanaume 25 wakiwa kila upande, na meli hiyo ingekuwa na urefu wa mita 30 na mlingoti wenye urefu wa mita 10.
Meli za Kivita za “Kitimu” Katika Unabii wa Biblia
Roho ya Yehova ndiyo iliyoongoza maneno haya: “Kutakuwako meli kutoka pwani ya Kitimu, nazo hakika zitatesa Ashuru.” (Hesabu 24:2, 24) Je, utabiri huo ulitimia? Meli kutoka Saiprasi zilihusika kwa njia gani katika utimizo huo? ‘Meli hizo kutoka pwani ya Kitimu’ hazikuwa za kufanya biashara ya amani katika Bahari ya Mediterania. Zilikuwa meli za vita zilizowaletea watu taabu.
Kadiri mahitaji ya kivita yalivyobadilika, ndivyo miundo ya msingi ya meli ilivyobadilishwa ili kutokeza meli ambazo zingeendeshwa haraka zaidi na zenye nguvu zaidi. Huenda meli za kivita za mapema zaidi za Saiprasi zilikuwa katika mchoro uliopatikana huko Amathus. Meli hiyo ni nyembamba na ndefu nayo ina tezi iliyoinuka na kujipinda kuelekea ndani ya meli, kama meli ya vita ya Foinike. Ina mdomo wa kutoboa meli ya adui na ngao za mviringo pande zote mbili za tezi na kuelekea omo ya meli hiyo.
-
-
“Meli za Kitimu” Zatawala BahariniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
Wasaiprasi walimuunga mkono Aleksanda Mkuu alipozingira Tiro (332 K.W.K.), kwa kumpa meli 120. Wafalme watatu wa Saiprasi waliziongoza meli hizo kwenda kujiunga na Aleksanda. Walishiriki kulizingira Tiro kwa muda wa miezi saba. Tiro lilianguka, na unabii wa Biblia ukatimia. (Ezekieli 26:3, 4; Zekaria 9:3, 4) Aleksanda aliwashukuru wafalme wa Saiprasi kwa kuwapa mamlaka ya pekee.
Utimizo Wenye Kustaajabisha
Strabo, mwanahistoria wa karne ya kwanza, anasema kwamba Aleksanda aliomba meli kutoka Saiprasi na Foinike ili azitumie katika harakati zake za kuingia Arabia. Meli hizo zilikuwa nyepesi na zingeweza kubomolewa kwa urahisi, hivyo ilichukua siku saba tu kuzifikisha Thapsacus (Tiphsah), kaskazini mwa Siria. (1 Wafalme 4:24) Kutoka hapo ilikuwa rahisi kushuka kwenda Babiloni zikifuata mto.
-
-
“Meli za Kitimu” Zatawala BahariniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 17]
Meli ya Saiprasi kwenye chombo cha maua
[Hisani]
Published by permission of the Director of Antiquities and the Cyprus Museum
-