Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Hutangaza “Tangu Mwanzo Ule Mwisho”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 1
    • 1, 2. Ni jambo gani la ajabu kuhusu matukio yanayohusiana na kuangushwa kwa Babiloni, nalo linaonyesha nini kumhusu Yehova?

      NI USIKU. Maaskari adui wananyemelea kupitia Mto Efrati huku wakielekea kwenye shabaha yao, jiji kuu la Babiloni. Wanapokaribia lango la jiji, wanaona jambo la kushangaza. Malango mawili kwenye ukuta wa Babiloni yameachwa wazi! Maaskari hao wanapanda kutoka mtoni, kisha wanaingia jijini. Kufumba na kufumbua, jiji hilo linatekwa. Bila kukawia, kiongozi wa maaskari hao anayeitwa Koreshi anaanza kusimamia eneo hilo lililotekwa, na baadaye anaagiza kwamba mateka Waisraeli waachiliwe huru. Maelfu ya watu walio uhamishoni wanarudi nyumbani kurudisha ibada ya Yehova huko Yerusalemu.—2 Mambo ya Nyakati 36:22, 23; Ezra 1:1-4.

      2 Wanahistoria wanaunga mkono kabisa matukio hayo ya mwaka wa 539-537 K.W.K. Jambo la ajabu ni kwamba matukio hayo yalijulikana karibu miaka 200 mapema. Kupitia roho yake, Yehova alimwongoza nabii wake Isaya afafanue mapema hivyo kuhusu kuanguka kwa Babiloni. (Isaya 44:24–45:7) Mungu hakufunua tu mambo yaliyohusiana na kuangushwa kwa Babiloni, bali pia alitaja jina la kiongozi wa mashambulizi hayo.a

  • Yehova Hutangaza “Tangu Mwanzo Ule Mwisho”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 1
    • 6. “Shauri” la Yehova lilitimiaje kuhusiana na kuanguka kwa Babiloni?

      6 Yehova alisema hivi kupitia nabii wake Isaya: “Shauri langu mwenyewe litasimama, na kila jambo ambalo ni mapenzi yangu nitafanya.” (Isaya 46:10b) “Shauri” la Mungu, yaani, mapenzi yake au kusudi lake kuhusu Babiloni, lilihusisha kumwita Koreshi kutoka Uajemi ili ashinde Babiloni na kuliangusha. Yehova alitangaza kusudi hilo miaka mingi mapema. Kama tulivyotaja tayari, kusudi hilo lilitimia mwaka wa 539 K.W.K.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki