-
Arusi Zenye Shangwe Zinazomletea Yehova HeshimaMnara wa Mlinzi—2000 | Mei 1
-
-
Inaelekea kwamba kulikuwa na muziki ufaao na watu walicheza dansi kwa adabu kwa sababu ilikuwa kawaida kuwa na dansi katika vikusanyiko vya Wayahudi. Yesu alionyesha jambo hilo katika mfano wake maarufu wa mwana mpotevu. Baba tajiri katika hadithi hiyo alifurahi sana kuona mwana wake aliyetubu amerudi hivi kwamba alisema: “Acheni tule na kujifurahisha wenyewe.” Kulingana na Yesu, sherehe hiyo ilitia ndani “utumbuizo wa kimuziki na uchezaji-dansi.”—Luka 15:23, 25.
Hata hivyo, ni jambo la kutokeza kwamba Biblia haitaji muziki wala kucheza dansi kwenye arusi ya Kana. Hata dansi haitajwi katika masimulizi yoyote ya arusi katika Biblia. Basi inaonekana kwamba miongoni mwa watumishi waaminifu wa Mungu wa nyakati za Biblia, dansi ingetukia lakini haikuwa sehemu kuu ya arusi zao. Je, tunaweza kujifunza jambo kutokana na mambo hayo?
Katika arusi fulani za Wakristo huku Afrika, vyombo vyenye nguvu sana vya muziki hutumiwa. Muziki waweza kuwa wenye sauti kubwa sana hivi kwamba wageni hawawezi kuzungumza kwa starehe. Nyakati nyingine inakuwa wazi kwamba chakula kimepungua lakini dansi ambayo inaweza kupita kiasi kwa urahisi haipungui. Badala ya kuwa sherehe ya arusi, pindi kama hizo zaweza kuwa tu udhuru wa kucheza dansi. Isitoshe, mara nyingi muziki wenye sauti kubwa huwavutia watu wenye fujo ambao huja bila kualikwa.
Kwa kuwa masimulizi ya Biblia ya arusi hayasisitizi muziki na dansi, je, jambo hilo halipasi kuwaongoza wale wanaopanga kufanya arusi ambayo itamletea Yehova heshima? Na wakati wa kufanya matayarisho ya arusi kadhaa za hivi majuzi katika sehemu ya kusini mwa Afrika, vijana Wakristo waliochaguliwa kuwa katika msafara wa arusi walitumia muda wa saa nyingi sana wakifanya mazoezi magumu ya dansi watakazocheza. Kwa miezi kadhaa wakati mwingi sana ulitumiwa kufanya mazoezi hayo. Lakini Wakristo wanahitaji ‘kununua kabisa wakati’ kwa ajili ya “mambo yaliyo ya maana zaidi,” kama vile kazi ya kueneza evanjeli, funzo la binafsi, na kuhudhuria mikutano ya Kikristo.—Waefeso 5:16; Wafilipi 1:10.
-
-
Arusi Zenye Shangwe Zinazomletea Yehova HeshimaMnara wa Mlinzi—2000 | Mei 1
-
-
Ikiwa watu watacheza dansi, wanaweza kucheza kwa utaratibu na kwa adabu. Watu wa ukoo ambao si waamini au Wakristo ambao hawajakomaa wakicheza dansi kwa njia chafu ya kukosa adabu au kwa njia ya kuamsha tamaa ya ngono, bwana-arusi anaweza kubadili muziki huo au kwa busara kukomesha dansi hiyo. La sivyo, arusi hiyo inaweza kuharibika na kuwa yenye fujo na ikwaze watu.—Waroma 14:21.
Kwa sababu kuna hatari katika dansi fulani za siku hizi, muziki wenye sauti kubwa, na pombe nyingi, mabwana-arusi wengine Wakristo wameamua kutopangia mambo hayo katika arusi yao. Mabwana-arusi wengine wameshutumiwa kwa kufanya hivyo, lakini wao wanapasa kupongezwa kwa kutaka kuepuka chochote ambacho huenda kikaletea suto jina takatifu la Mungu. Kwa upande mwingine, mabwana-arusi wengine hupanga kuwe na muziki ufaao, wakati wa kucheza dansi, na kuandaa pombe kwa kiasi. Kwa vyovyote vile, bwana-arusi anawajibika kwa mambo anayoyaruhusu katika arusi yake.
-