Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • “UTASIMAMA”

      18, 19. (a) Malaika alimaanisha nini alipomwambia Danieli kwamba ‘angesimama’ wakati ujao? (b) Danieli angewezaje kujua juu ya tumaini la ufufuo?

      18 Kitabu cha Danieli chamalizika kwa mojawapo ya ahadi nzuri sana ambazo Mungu amepata kumwahidi mwanadamu. Malaika wa Yehova alimwambia Danieli hivi: “Nawe utasimama katika kura yako mwisho wa siku hizo.” Malaika huyo alimaanisha nini? Basi, kwa kuwa ‘starehe’ aliyokuwa ametoka tu kurejezea ilikuwa kifo, ahadi ya kwamba Danieli ‘angesimama’ wakati fulani ujao, ingeweza kumaanisha kitu kimoja tu—ufufuo!b Hata wasomi fulani wamesisitiza kwamba Danieli sura ya 12 ina rejezo la kwanza lililo wazi kabisa juu ya ufufuo liwezalo kupatikana katika Maandiko ya Kiebrania. (Danieli 12:2) Hata hivyo, wamekosea. Danieli alijua vema juu ya tumaini la ufufuo.

      19 Kwa kielelezo, haikosi Danieli alijua maneno haya ambayo Isaya alikuwa amerekodi karne mbili mapema: “Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana . . . ardhi itawatoa waliokufa.” (Isaya 26:19) Muda mrefu kabla ya hapo, Eliya na Elisha waliwezeshwa na Yehova kufufua watu kihalisi. (1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:32-37) Hata mapema zaidi, Hana, mama ya nabii Samweli, alikiri kwamba Yehova aweza kuleta watu juu kutoka kuzimu, kaburini. (1 Samweli 2:6) Isitoshe, hata mapema zaidi, Yobu mwaminifu alionyesha tumaini lake mwenyewe katika maneno haya: “Mtu akifa, je! atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, hata kufunguliwa kwangu kunifikilie. Wewe ungeita, nami ningekujibu; ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.”—Ayubu 14:14, 15.

      20, 21. (a) Kwa hakika Danieli atapata ufufuo gani? (b) Yamkini ufufuo katika Paradiso utafanywaje?

      20 Kama Yobu, Danieli alikuwa na sababu za kuwa na uhakika kwamba Yehova kwa kweli angetamani sana kumrudisha kwenye uhai siku fulani wakati ujao. Hata hivyo, bado lazima alitiwa moyo sana kusikia kiumbe-roho chenye nguvu kikimhakikishia tumaini hilo. Ndiyo, Danieli atasimama katika “ufufuo wa walio waadilifu,” utakaofanywa wakati wa Utawala wa Mileani wa Kristo. (Luka 14:14) Hilo litakuwaje kwa Danieli? Neno la Mungu hutuambia mengi zaidi juu yake.

  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • b Kulingana na The Brown-Driver-Briggs Hebrew and English Lexicon, neno la Kiebrania linalotafsiriwa “-simama” ambalo latumiwa hapa larejezea “kuhuishwa baada ya kifo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki