-
Kutayarisha Kwa Ajili Ya Ndoa Yenye MafanikioSiri ya Furaha ya Familia
-
-
11, 12. Watu wawili waweza kujuaje kama wao wanafaana au la?
11 Je, ni desturi mahali unapoishi mtu kujichagulia mwenzi wake mwenyewe wa ndoa? Ikiwa ndivyo, basi, uchukue hatua gani ikiwa wampata mtu fulani wa jinsia tofauti kuwa mwenye kuvutia? Kwanza, jiulize mwenyewe, ‘Je, kweli kusudi langu ni kufunga ndoa?’ Ni jambo la kikatili kuchezea hisiamoyo za mtu mwingine kwa kutokeza matazamio yasiyo ya kweli. (Mithali 13:12) Kisha, jiulize, ‘Je, niko tayari kufunga ndoa?’ Ikiwa jibu kwa maswali hayo mawili ni ndiyo, hatua zifuatazo utakazochukua zitakuwa tofauti kwa kutegemea desturi za kwenu.
-
-
Kutayarisha Kwa Ajili Ya Ndoa Yenye MafanikioSiri ya Furaha ya Familia
-
-
13. Kwa nini ni jambo linalokosa hekima sana kutafuta uchumba na mtu ambaye hashiriki imani yako?
13 Ni jambo la maana kwamba nyote wawili mwe na itikadi na kanuni zilezile. Mtume Paulo aliandika hivi: “Msiwe wenye kufungwa nira isiyosawazika pamoja na wasio waamini.” (2 Wakorintho 6:14; 1 Wakorintho 7:39) Ndoa pamoja na mtu ambaye hashiriki imani yako katika Mungu hufanya iwe yamkini zaidi kwamba kutakuwa na hali mbaya ya kutopatana. Kwa upande ule mwingine, ujitoaji wa wote wawili kwa Yehova Mungu ndio msingi ulio imara zaidi sana wa kuwa na muungano. Yehova akutaka uwe na furaha na ufurahie kifungo cha karibu zaidi iwezekanavyo pamoja na mtu ambaye unafunga ndoa naye. Yeye ataka mfunganishwe kwake Yeye na kwa nyinyi kwa nyinyi kwa kifungo cha upendo chenye nyuzi tatu.—Mhubiri 4:12.
-