Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Msamaha wa Yehova Unamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Novemba 15
    • SALA YA DAUDI NA MSAMAHA WA MUNGU

      8, 9. Zaburi ya 51 inafunuaje hisia za moyoni za Daudi, na inatufundisha nini kumhusu Yehova?

      8 Maneno ya wimbo ambao Mfalme Daudi alitunga baadaye yanafunua jinsi alivyojuta kutoka moyoni. Zaburi ya 51 ina sihi zenye kugusa moyo ambazo Daudi alimtolea Yehova na inaonyesha wazi kwamba alifanya mengi zaidi kuliko kukiri tu makosa yake. Alitubu pia dhambi zake. Daudi alihangaikia hasa uhusiano wake na Mungu. Aliungama hivi: “Dhidi yako wewe, wewe peke yako, nimetenda dhambi.” Akamsihi Yehova: “Uumbe moyo safi ndani yangu, Ee Mungu, na kuweka ndani yangu roho mpya, iliyo imara. . . . Unirudishie shangwe ya wokovu wako, nawe unitegemeze kwa roho ya kupenda.” (Zab. 51:1-4, 7-12) Je, wewe pia unazungumza na Yehova kwa unyoofu na kwa bidii kuhusu makosa yako?

  • Msamaha wa Yehova Unamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Novemba 15
    • Kama Yesu alivyoeleza, Yehova anatutendea kama tunavyowatendea wengine. Yesu alisema hivi: “Acheni kuhukumu ili msihukumiwe; kwa maana kwa hukumu mnayohukumu, mtahukumiwa; na kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi.” (Mt. 7:1, 2) Inafariji kama nini kujua kwamba Yehova atatusamehe dhambi zetu, hata dhambi nzito kama vile uzinzi au uuaji! Atatusamehe tukiwa na roho ya kusamehe, tukiungama dhambi zetu mbele yake, na tukionyesha kwamba tumebadili mtazamo wetu kuelekea matendo yetu mabaya. Watenda-dhambi wanapotubu kikweli wanapata “majira ya kuburudisha” kutoka kwa Yehova.​—Soma Matendo 3:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki