-
Mungu Anamchagua DaudiKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 57
Mungu Anamchagua Daudi
UNAWEZA kuona yaliyotokea? Mvulana huyu amemwokoa mwana-kondoo mdogo asiliwe na dubu. Dubu huyo alikuja akamchukua mwana-kondoo amle. Lakini mvulana huyo akafuatia, akamwokoa mwana-kondoo katika kinywa cha dubu. Dubu aliporukia mvulana, alimkamata na kumwua! Wakati mwingine aliokoa kondoo mmoja asiliwe na simba. Je! huyo si mvulana hodari? Unajua ni nani?
Ni kijana Daudi. Anakaa katika mji wa Bethlehemu. Babu yake ni Obedi, mwana wa Ruthu na Boazi. Unawakumbuka? Baba ya Daudi ni Yese. Daudi anachunga kondoo za baba yake. Daudi alizaliwa miaka 10 baada ya Yehova kuchagua Sauli awe mfalme.
Unafika wakati Yehova anapomwambia Samweli hivi: ‘Chukua mafuta ya pekee uende nyumbani kwa Yese huko Bethlehemu. Nimechagua mmoja kati ya wanawe awe mfalme.’ Samweli anapomwona Eliabu mwana mkubwa wa Yese, anasema hivi: ‘Bila shaka huyu ndiye Yehova amechagua.’ Lakini Yehova anamwambia: ‘Usitazame urefu na uzuri wake. Sikumchagua awe mfalme.’
Basi Yese anamwita Abinadabu mwanawe na kumpeleka kwa Samweli. Lakini Samweli anasema: ‘Hapana, Yehova hakumchagua wala huyu.’ Tena, Yese amleta Shama mwanawe. ‘Hapana, Yehova hakuchagua wala huyu,’ asema Samweli. Yese ampelekea Samweli wanawe saba, lakini Yehova hachagui yeyote kati yao. ‘Je! wavulana ni hawa tu?’ Samweli auliza.
‘Bado kuna mdogo wao,’ Yese asema. ‘Lakini yeye anachunga kondoo.’ Daudi anapoingizwa, Samweli anamwona kuwa kivulana mzuri. ‘Huyu ndiye,’ Yehova asema. ‘Mmwagie mafuta.’ Samweli anafanya hivyo. Utafika wakati Daudi atakapokuwa mfalme wa Israeli.
-
-
Daudi na GoliathiKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 58
Daudi Na Goliathi
TENA Wafilisti wanakuja kupigana na Israeli. Wakati huu ndugu zake Daudi wakubwa watatu wamo katika jeshi la Sauli. Basi siku moja Yese amwambia Daudi hivi: ‘Wapelekee ndugu zako nafaka na mikate. Kaone kama ni wazima.’
Daudi anapofika kwenye kambi ya jeshi, anapiga mbio kwenda kwenye mapigano akawatafute ndugu zake. Goliathi (Goliata), jitu la Wafilisti anajitokeza ili awacheke Waisraeli. Kwa muda wa siku 40 amekuwa akifanya hivyo asubuhi na jioni. Anapaza sauti: ‘Haya, chagueni mmoja apigane nami.’
Daudi anauliza askari fulani hivi: ‘Atapata nini mtu anayemwua Mfilisti huyu na kuwaondolea Waisraeli aibu hii?’
‘Sauli atampa mtu huyo mali nyingi,’ askari anasema. ‘Naye atampa binti yake awe mke wake.’
Lakini Waisraeli wote wanamwogopa Goliathi kwa sababu ni mkubwa mno. Urefu wake ni zaidi ya mita tatu, na ana askari mwingine wa kumchukulia ngao.
Askari fulani wanakwenda kumwambia Mfalme Sauli kwamba Daudi anataka kupigana na Goliathi. Lakini Sauli anamwambia Daudi hivi: ‘Wewe huwezi kupigana na Mfilisti huyu. Wewe ni mtoto tu, yeye amekuwa askari maisha yake yote.’ Daudi anajibu hivi: ‘Mimi niliua dubu na simba aliyechukua kondoo wa baba. Na Mfilisti huyu atakuwa kama huyo. Yehova atanisaidia.’ Basi Sauli anasema: ‘Nenda, Yehova awe nawe.’
Daudi anatelemkia njia ya kijito na kuchagua mawe matano laini, na kuyaweka mfukoni mwake. Kisha anachukua kombeo lake na kwenda kukutana na jitu lile. Goliathi anapomwona anamdharau. Anadhani itakuwa rahisi sana kumwua Daudi.
‘Wewe njoo tu kwangu,’ Goliathi asema, ‘nami nitawapa ndege na wanyama wapate kula mwili wako.’ Lakini Daudi anasema: ‘Wewe unakuja kwangu kwa upanga na mkuki, lakini mimi ninakuja kwako kwa jina la Yehova. Leo hii Yehova atakutia wewe mikononi mwangu nami nitakuangusha chini.’
Papo hapo Daudi anamkimbilia Goliathi. Anachukua jiwe katika mfuko wake, analiweka katika kombeo lake, na kulitupa kwa nguvu zake zote. Jiwe hilo linaingia moja kwa moja kichwani mwa Goliathi, anaanguka na kufa! Wafilisti wanapoona bingwa wao ameanguka, wote wanageuka na kukimbia. Waisraeli wanawafuatia mbio na kushinda vita.
-
-
Sababu Yampasa Daudi AkimbieKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 59
Sababu Yampasa Daudi Akimbie
BAADA ya Daudi kumwua Goliathi, Abneri mkuu wa jeshi anampeleka kwa Sauli. Sauli anapendezwa sana na Daudi. Anamfanya mkuu katika jeshi lake na kumchukua akakae katika nyumba ya mfalme.
Baadaye, jeshi linaporudi kupigana na Wafilisti, wanawake wanaimba hivi: ‘Sauli ameua maelfu, lakini Daudi makumi ya maelfu.’ Hilo lamfanya Sauli aone wivu, kwa sababu Daudi anaheshimiwa kuliko Sauli. Lakini Yonathani mwana wa Sauli haoni wivu. Anampenda Daudi sana, naye Daudi anampenda Yonathani pia. Hao wawili wanapeana ahadi kwamba watakuwa rafiki sikuzote.
Daudi anajua sana kupiga kinubi, naye Sauli anapenda muziki anaopiga Daudi. Lakini siku moja wivu wa Sauli wamfanya atende jambo baya. Wakati Daudi anapopiga kinubi, Sauli anachukua mkuki wake na kuutupa, akisema: ‘Nitampigilia Daudi ukutani!’ Lakini Daudi apiga chenga (aepa), na mkuki wamkosa. Baadaye Sauli akosa tena kumpiga Daudi kwa mkuki wake. Basi Daudi anajua yampasa awe mwangalifu sana.
Unajua ahadi ya Sauli! Alisema angetoa binti yake awe mke wa yule mtu ambaye angeua Goliathi. Mwishowe Sauli anamwambia Daudi achukue Mikali binti yake, lakini kwanza yampasa aue Wafilisti adui 100. Ebu wazia hilo! Sauli anatumaini kwamba Wafilisti watamwua Daudi. Lakini hawamwui, hivyo Sauli anampa Daudi binti yake awe mke wake.
Siku moja Sauli anamwambia Yonathani na watumishi wake wote kwamba anataka kumwua Daudi. Lakini Yonathani anamwambia babaye hivi: ‘Usimwumize Daudi. Hajakukosea. Kila alichofanya kimekuwa msaada mkubwa kwako. Aliweka uhai wake katika hatari alipomwua Goliathi, na ulipoona, ukafurahi.’
Sauli amsikiliza mwanawe, na kuahidi asimwumize Daudi. Daudi anarudishwa, naye anamtumikia Sauli tena nyumbani mwake kama zamani. Lakini, siku moja wakati Daudi anapopiga muziki, Sauli anamtupia Daudi mkuki wake tena. Daudi apiga chenga, mkuki unapiga ukuta. Hii ndiyo mara ya tatu! Sasa Daudi ajua yampasa akimbie!
Usiku huo Daudi aenda nyumbani kwake. Lakini Sauli anatuma watu fulani wakamwue. Mikali anajua mipango ya baba yake. Anamwambia mume wake hivi: ‘Usipoondoka usiku huu, kesho utakuwa umekufa.’ Inampasa Daudi ajifiche hapa na pale muda wa karibu miaka saba, Sauli asimwone.
-
-
Abigaili na DaudiKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 60
Abigaili na Daudi
JE! UNAMJUA mwanamke huyu mzuri anayekuja kumlaki Daudi? Jina lake ni Abigaili. Ni mwenye akili nzuri, naye anamzuia Daudi asifanye ubaya. Lakini kabla ya kujifunza hayo, tuone ni mambo gani yamekuwa yakimpata Daudi.
Daudi akiisha kumkimbia Sauli, anajificha katika pango. Ndugu zake na wengine wa jamaa yake wanajiunga naye huko. Karibu jumla ya watu 400 wanamwendea, Daudi anakuwa kiongozi wao. Kisha Daudi anamwendea mfalme wa Moabu na kusema: ‘Tafadhali ruhusu baba na mama yangu wakae nawe mpaka nione yatakayonipata.’ Baadaye Daudi na watu wake wanaanza kujificha vilimani.
Ni baada ya hayo kwamba Daudi akutana na Abigaili. Nabali mume wake ni mtu tajiri mwenye mashamba. Ana kondoo 3,000 na mbuzi 1,000. Nabali ni mchoyo. Lakini Abigaili mkewe ni mwenye sura nzuri sana. Pia, anajua kutenda mema. Wakati mmoja hata aliokoa jamaa yake. Na tuone ilivyokuwa.
Daudi na watu wake wamemtendea mema Nabali. Wamelinda kondoo zake. Basi siku moja Daudi anatuma watu wake wakamwombe Nabali awasaidie. Watu wa Daudi wanamwendea Nabali wakati yeye na wasaidizi wake wanakata manyoya ya kondoo. Ni siku ya karamu, naye Nabali ana chakula kingi kizuri. Basi watu wa Daudi wanamwambia hivi: ‘Sisi tumekutendea mema. Hatukuiba kondoo wako ye yote, ila tumesaidia kuwachunga. Basi, tafadhali, utupe chakula kidogo.’
‘Siwezi kuwapa chakula watu kama ninyi,’ Nabali anasema. Anasema kwa njia mbaya sana, na kumtukana Daudi. Watu hao wanaporudi na kumwambia Daudi, Daudi anakasirika sana. ‘Jivikeni panga zenu!’ awaambia watu wake. Nao wanaanza safari kwenda kuua Nabali na watu wake.
Mmoja wa watu wa Nabali, waliosikia matusi ya Nabali, anamwambia Abigaili yaliyotokea. Mara hiyo Abigaili anatayarisha chakula. Anakiweka juu ya punda wake, anapokutana na Daudi njiani, ainama na kusema: ‘Tafadhali, bwana, usimwangalie mume wangu yule Nabali. Yeye ni mpumbavu, anafanya mapumbavu. Hii ni zawadi. Tafadhali ichukue, utusamehe yaliyotokea.’
‘Wewe ni mwanamke mwenye akili,’ Daudi ajibu. ‘Umenizuia nisimwue Nabali na kumlipa kwa choyo yake. Basi nenda zako kwa amani.’ Baadaye, Nabali anapokufa, Abigaili anakuwa mke wa Daudi.
-
-
Daudi Anafanywa MfalmeKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 61
Daudi Anafanywa Mfalme
TENA Sauli anajaribu kumkamata Daudi. Anachukua askari wake bora zaidi 3,000 na kwenda kumtafuta. Daudi anapojua hivyo, anatuma wapelelezi ajue mahali ambapo Sauli na watu wake wamepiga kambi walale usiku. Ndipo Daudi anawaambia watu wake hivi: ‘Ni nani atakayekwenda pamoja nami kenye kambi ya Sauli?’
‘Mimi,’ Abishai anajibu. Abishai ni mwana wa Seruya dada yake Daudi. Wakati Sauli na watu wake wamelala, Daudi na Abishai wanaingia kambini kimya-kimya. Wanachukua mkuki na mtungi wa Sauli. Hakuna mtu anayeona wala kuwasikia kwa sababu wote wamelala sana.
Ebu mwone sasa Daudi na Abishai. Wamekwisha kwenda mbali, nao wako salama juu ya kilima. Daudi anampazia sauti mkuu wa jeshi la Israeli hivi: ‘We-e Abneri, sababu gani humlinda bwanako, mfalme? Tazama! Mkuki na mtungi wake viko wapi?’
Sauli anaamka. Aitambua sauti ya Daudi, kisha auliza: ‘Ni wewe, Daudi?’ Unaweza kumona Sauli na Abneri chini kule?
‘Ndiyo, bwanangu mfalme,’ Daudi amjibu Sauli. Naye Daudi auliza hivi: ‘Kwa nini wataka kunikamata? Nimefanya ubaya gani? Mkuki wako huu, Ee mfalme. Mtume mmoja wa watu wako aje auchukue.’
‘Nimekosa,’ Sauli anakubali. ‘Nimetenda kipumbavu.’ Ndipo Daudi anakwenda zake, naye Sauli anarudi kwake. Lakini Daudi anajisemesha hivi: ‘Siku fulani Sauli ataniua mimi. Yanipasa nikimbie niende kwenye nchi ya Wafilisti.’ Anafanya hivyo. Daudi anapumbaza Wafilisti na kuwafanya waamini yuko upande wao.
Wakati fulani baadaye Wafilisti wanakwenda kupigana na Israeli. Huko vitani, Sauli na Yonathani wanauawa. Hilo lamhuzunisha Daudi sana, naye anaandika wimbo mzuri, akiimba hivi: ‘Naona huzuni kwa ajili yako, ndugu yangu Yonathani. Jinsi nilivyokupenda!’
Baada ya hayo Daudi anarudi Israeli kwenye mji Hebroni. Kwatokea vita kati ya watu wanaochagua Ishboshethi mwana wa Sauli, awe mfalme, na watu wegine wanaotaka Daudi awe mfalme. Lakini Mwishowe watu wa Daudi wanashinda. Sasa Daudi ni mwenye miaka 30 anapofanywa kuwa mfalme. Anatawala katika Hebroni kwa miaka saba na nusu.
Wakati wafika wa Daudi na watu wake kwenda kuteka mji mzuri unaoitwa Yerusalemu. Yoabu, mwana mwingine wa Seruya, dada yake Daudi, anaongoza vita. Basi Daudi anamfanya Yoabu kuwa mkuu wa jeshi lake. Sasa Daudi anaanza kutawala katika mji wa Yerusalemu.
-
-
Matata Katika Nyumba ya DaudiKitabu Changu cha Hadithi za Biblia
-
-
HADITHI YA 62
Matata Katika Nyumba ya Daudi
BAADA ya Daudi kuanza kutawala katika Yerusalemu, Yehova analipa jeshi lake ushindi mwingi juu ya adui zao. Yehova alikuwa ameahidi kuwapa Waisraeli nchi ya Kanaani. Na sasa, kwa msaada wa Yehova, nchi yote waliyoahidiwa inakuwa yao.
Daudi ni mtawala mzuri. Anampenda Yehova. Basi baada ya kuuteka Yerusalemu, kwanza anapeleka sanduku la agano huko. Tena anataka kujenga hekalu aweke sanduku humo.
Daudi anapokuwa mzee kidogo, anafanya kosa baya. Daudi anajua kwamba ni vibaya kuchukua kitu cha mwingine. Lakini usiku mmoja, anapokuwa katika dari ya jumba lake la kifalme, anamwona mwanamke mzuri sana. Jina lake ni Bath-sheba, na mume wake ni Uriya, mmoja wa askari zake.
Daudi anamtaka Bath-sheba sana sana. Basi anaagiza aletwe kwenye jumba lake la kifalme. Mume wake amekwenda vitani. Daudi analala naye, kisha anaona amepata mimba. Daudi anapata wasiwasi mwingi. Anampelekea Yoabu mkuu wa jeshi ujumbe ili Uriya awekwe mbele ya pigano ambapo atauawa. Uriya anapokufa, Daudi anamwoa Bath-sheba.
Yehova anamkasirikia Daudi sana. Anamtuma Nathani mtumishi wake akamwambie dhambi zake. Unamwona hapa Nathani akizungumza na Daudi. Daudi anatubu makosa aliyofanya, kwa hiyo Yehova hamwui. Lakini Yehova anasema: ‘Kwa kuwa umefanya mabaya haya, utakuwa na matata mengi nyumbani mwako.’ Na Daudi anapata matata wee!
Kwanza, mwana wa Bath-sheba anakufa. Kisha Am’noni mzaliwa wa kwanza wa Daudi amchukua Tamari dada yake wakiwa peke yao na kumlala kinguvu. Absalomu mwana wa Daudi anakasirika sana hata anamwua Am’noni. Baadaye, Absalomu anapendwa na watu wengi, na kujifanya mfalme. Mwishowe, Daudi anashinda Absalomu katika kupigana, naye auawa. Ndiyo, Daudi amepata matata mengi.
Wakati huo, Bath-sheba anazaa mwana mwingine jina lake Sulemani. Daudi anapokuwa mzee na mgonjwa, Adoniya mwanawe, anataka kujifanya mfalme. Kwa hiyo Daudi anaagiza kuhani Sadoki amwage mafuta kichwani pa Sulemani, kuonyesha kwamba Sulemani atakuwa mfalme. Mara baada ya hayo, Daudi anakufa akiwa na miaka 70. Alitawala kwa miaka 40, lakini sasa Sulemani ndiye mfalme wa Israeli.
-