-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Akiwa kijana, Daudi wa Israeli la kale alikabili majaribu pia. Kwa muda wa miaka mingi, alilazimika kuishi kama mtoro, akiwindwa kama mnyama na Mfalme Sauli. Maisha ya Daudi yalikuwa hatarini sikuzote. Wakati mmoja, alienda kwa kuhani Ahimeleki ili kuomba chakula. (1 Samweli 21:1-7) Sauli aliposikia kwamba Ahimeleki alikuwa amemsaidia Daudi, aliagiza Ahimeleki, makuhani wote, na familia zao, wauawe. (1 Samweli 22:12-19) Je, unaweza kuwazia uchungu ambao Daudi alihisi moyoni kwa kusababisha kwa njia isiyo ya moja kwa moja msiba huo?
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Vivyo hivyo, Daudi hakumfungia kinyongo Mfalme Sauli. Daudi alipata nafasi mbili za kumuua Sauli. Hata hivyo, wanaume wake walipomhimiza amuue, Daudi alisema: “Ni jambo lisilowaziwa kwangu, kwa maoni ya Yehova, kwamba nimfanyie bwana wangu jambo hili, mtiwa-mafuta wa Yehova, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mtiwa-mafuta wa Yehova.” Daudi aliacha Yehova asuluhishe mambo, kwa kuwaambia wanaume wake hivi: “Kama Yehova anavyoishi, Yehova mwenyewe atampiga; au siku yake itakuja naye atakufa, au ataanguka vitani, na kufagiliwa mbali.” Baadaye, Daudi hata alitunga wimbo wa maombolezo kwa ajili ya Sauli na mwanaye Yonathani. Kama vile Yosefu, Daudi hakujiacha ashindwe na kinyongo.—1 Samweli 24:3-6; 26:7-13; 2 Samweli 1:17-27.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Katika miaka ambayo Daudi aliishi kama mtoro, yeye pia alijitahidi kadiri alivyoweza kulingana na hali zake. Walipokuwa wakiishi katika nyika ya Parani, yeye na wanaume wake walilinda mifugo ya Nabali isiporwe na vikundi vya waporaji. “Walikuwa ukuta kutuzunguka wakati wa usiku na wakati wa mchana,” akasema mmoja wa wachungaji wa Nabali. (1 Samweli 25:16) Baadaye, wakati alipokuwa Ziklagi, Daudi alivamia miji iliyokaliwa na maadui wa Israeli upande wa kusini, hivyo mipaka ya Yuda ikawa salama.—1 Samweli 27:8; 1 Mambo ya Nyakati 12:20-22.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Mngojee Yehova
Jambo la tatu la kujifunza ni kwamba badala ya kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kurekebisha hali zetu, tunapaswa kumngojea Yehova. Mwanafunzi Yakobo aliandika: “Acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yakobo 1:4) Tunapaswa kuacha uvumilivu “ukamilishe kazi yake” kwa kuvumilia majaribu hadi mwisho bila kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kuyakomesha upesi. Hivyo, imani yetu itajaribiwa na kusafishwa, na itafunuliwa kama imani yetu ina nguvu ya kututegemeza. Yosefu na Daudi walikuwa na uvumilivu wa aina hiyo. Hawakujaribu kutafuta suluhisho ambalo lingeweza kumkasirisha Yehova. Badala yake, walijitahidi kadiri walivyoweza kulingana na hali zao. Waliendelea kumngojea Yehova, nao wakapokea baraka nyingi sana kwa kufanya hivyo. Wote wawili walitumiwa na Yehova kuokoa na kuongoza watu wake.—Mwanzo 41:39-41; 45:5; 2 Samweli 5:4, 5.
-
-
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?Mnara wa Mlinzi—2004 | Juni 1
-
-
Yehova Atakutegemeza
Tunaweza kunufaika kwa kutafakari jinsi watu wanaotajwa na Biblia, kama vile Yosefu na Daudi, walivyofanikiwa kushughulika na hali ngumu na zenye kukatisha tamaa. Ingawa habari kuwahusu zinaelezwa katika kurasa chache tu za Biblia, majaribu yao yalidumu kwa miaka mingi. Jiulize hivi: ‘Watumishi hao wa Mungu walijifunzaje kukabili hali zao? Walidumishaje shangwe yao? Walipaswa kukuza sifa gani?’
-