Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtu Anayekubalika kwa Moyo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 1
    • Alitumia Wakati Wake Vizuri

      Mchungaji alitumia wakati wake mwingi akiwa ametulia na akiwa peke yake. Lakini Daudi hakuruhusu achoshwe na maisha hayo. Badala yake, hali hiyo ya utulivu ilimwezesha Daudi kupata nafasi nyingi za kutafakari. Inaonekana kwamba mambo fulani ambayo Daudi anataja katika zaburi zake aliyatafakari alipokuwa kijana. Je, ni wakati huo alipokuwa peke yake alipotafakari kuhusu mahali pa mwanadamu katika mpango wa Mungu na pia kuhusu uumbaji wenye kustaajabisha ulio mbinguni, yaani, jua, mwezi, na nyota, “kazi za vidole [vya Yehova]”? Je, ni katika mashamba yaliyokuwa Bethlehemu alipotafakari kuhusu ardhi yenye rutuba, mifugo na ng’ombe wa kulima, ndege na “wanyama wa porini”?—Zaburi 8:3-9; 19:1-6.

      Bila shaka, mambo ambayo Daudi alipitia akiwa mchungaji yalimfanya ajionee kwa njia iliyo wazi hata zaidi jinsi Yehova anavyowatendea watumishi wake waaminifu kwa wororo. Hivyo Daudi aliimba hivi: “Yehova ni Mchungaji wangu. Sitakosa chochote. Ananilaza katika malisho yenye majani mengi; ananiongoza kando ya mahali pa kupumzika palipo na maji ya kutosha. Hata ingawa ninatembea katika bonde lenye kivuli kizito, siogopi chochote kibaya, kwa maana wewe uko pamoja nami; fimbo yako na gongo lako ndivyo vitu vinavyonifariji.”—Zaburi 23:1, 2, 4.

      Huenda ukajiuliza mambo hayo yote, yanakuhusu jinsi gani? Jibu ni kwamba sababu moja iliyomfanya Daudi awe na uhusiano wa karibu na Yehova na kuitwa “mtu anayekubalika kwa moyo wake” ni kwamba alitafakari kwa uzito sana kazi za Yehova na uhusiano wake na Mungu. Je, wewe unaweza kuwa kama Daudi?

      Je, umewahi kusukumwa kumsifu na kumtukuza Muumba baada ya kuchunguza kwa makini kitu fulani alichoumba? Je, umewahi kuhisi moyo wako umejaa upendo kwa Yehova baada ya kuona sifa zake kupitia jinsi anavyoshughulika na wanadamu? Kwa kawaida, ili uwe na uthamini kama huo, unapaswa kusali kwa Yehova na utenge wakati wa kutafakari kwa utulivu Neno la Mungu na uumbaji wake. Kutafakari kwa njia hiyo kunaweza kukusaidia kumjua Yehova kwa undani zaidi—na hivyo kumpenda. Vijana kwa wazee wanaweza kuwa na pendeleo hilo. Inaelekea Daudi alikuwa na uhusiano wa karibu na Yehova tangu alipokuwa kijana.

  • Mtu Anayekubalika kwa Moyo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 1
    • Vyovyote vile, Daudi alikuwa na umri mdogo sana Yehova alipomchagua. Hata hivyo, inaonekana tayari Daudi alikuwa mtu wa kiroho sana. Inaelekea alikuwa na uhusiano wa karibu na Yehova, ambao alisitawisha kwa kutafakari mambo aliyojua kumhusu Mungu.

      Leo, vijana wanapaswa kutiwa moyo wafanye hivyo pia. Kwa hiyo, je, wazazi mnawatia moyo watoto wenu watafakari mambo ya kiroho, wathamini uumbaji wa Mungu, na kujifunza mambo ambayo Biblia inasema kumhusu Muumba? (Kumbukumbu la Torati 6:4-9) Nanyi vijana, je, mnafanya mambo hayo bila kusukumwa? Machapisho yanayotegemea Biblia kama vile magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!b yamekusudiwa kuwasaidia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki