-
Kitabu Chenye Mwongozo UnaotegemekaJinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha
-
-
Kwa mfano, mfikirie Daudi, mfalme Mwisraeli anayejulikana sana. Hadi hivi karibuni, Biblia peke yake ndiyo iliyotaja kwamba kulikuwa na mtu aliyeitwa Daudi. Ingawa wanahistoria mashuhuri wanakubali kwamba ni mtu halisi, watu wengine wanaotilia shaka wanasema kwamba ni mtu wa kuwaziwa tu aliyebuniwa na Wayahudi waliotaka kueneza mawazo yao. Lakini ukweli wa mambo ni nini?
Maandishi yanayotaja “Nyumba ya Daudi”
6 Mwaka wa 1993, maandishi yanayotaja “Nyumba ya Daudi” yalipatikana kwenye magofu ya jiji la kale la Dani, la Waisraeli. Maandishi hayo yalikuwa sehemu ya mnara wa ukumbusho ulioharibika wa karne ya tisa K.W.K. ulioonyesha jinsi maadui walivyowashinda Waisraeli. Ghafla maandishi mengine kando na Biblia yanayomtaja Daudi yakapatikana. Je, hilo lilikuwa jambo muhimu? Israel Finkelstein, wa Chuo Kikuu cha Tel Aviv, alisema hivi kuhusu ugunduzi huo: “Wazo la kwamba maandishi ya Biblia hayana msingi likakoma ghafla baada ya maandishi hayo yanayomtaja Daudi kupatikana.”
-