Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Sisi Huogopa Kifo?
    Amkeni!—2007 | Desemba
    • Je, “Mavumbi” Ndio Mwisho wa Mambo Yote?

      Katika kitabu cha Mhubiri kilichoandikwa miaka 3,000 iliyopita, Sulemani aliandika hivi: “Walio hai wanajua kwamba kifo kitawapata, lakini wafu hawajui lolote, nao hawana thawabu tena, kwa sababu hawana kumbukumbu tena. Upendo wao na chuki yao na wivu wao umekwisha.” Aliongeza kusema: “Chochote kilicho katika uwezo wa mkono wako, kifanye kwa nguvu zako zote, kwa kuwa hakuna kazi, wala wazo, wala ujuzi, wala hekima mahali pa wafu ambapo wewe unaenda.”—Mhubiri 9:5, 6, 10, The Bible in Basic English.

      Pia, Sulemani akiongozwa na roho alisema kwamba “mwisho wa binadamu na mwisho wa mnyama ni uleule. Jinsi anavyokufa binadamu ndivyo anavyokufa mnyama. . . . binadamu si bora kuliko mnyama. . . . Wote hufa na kwenda mahali pamoja. Wote wametoka mavumbini, na wote watarudi mavumbini.”—Mhubiri 3:19, 20, Biblia Habari Njema.

      Ingawa maneno hayo yaliyoonyeshwa juu yaliandikwa na Mfalme Sulemani, yaliongozwa na roho ya Mungu na ni sehemu ya Biblia, Neno lake lililoandikwa. Maandiko hayo, pamoja na mengine mengi katika Biblia, hayaungi mkono imani ambayo watu wengi wanayo kwamba kitu fulani ndani yetu huendelea kuishi katika umbo fulani baada ya sisi kufa. (Mwanzo 2:7; 3:19; Ezekieli 18:4)

  • Je, Kweli Kifo Ndio Mwisho?
    Amkeni!—2007 | Desemba
    • Ulikuwa Katika Hali Gani Kabla ya Kuzaliwa?

      Kwa mfano, fikiria maandiko mawili ya Mfalme Sulemani yaliyonukuliwa katika makala iliyotangulia. Maandiko hayo yanaonyesha wazi kwamba wafu hawajui lolote kamwe, iwe ni wanadamu au wanyama. Hivyo, kulingana na Biblia, hakuna utendaji, ujuzi, hisia, au mawazo katika kifo.—Mhubiri 9:5, 6, 10.

      Je, ni vigumu kuelewa jambo hilo? Hebu fikiria: Mtu alikuwa katika hali gani kabla ya kuwa hai? Ulikuwa wapi kabla ya chembe ndogo za wazazi wako kuungana na kutokeza mtu hai, yaani, wewe? Ikiwa mwanadamu ana kitu fulani kisichoonekana ambacho huendelea kuishi baada ya mtu kufa, kitu hicho huwa wapi kabla ya chembe hizo za wazazi wako kuungana? Ukweli ni kwamba, hukuwepo kabla ya kuwa mwanadamu kwa hiyo huna kumbukumbu lolote. Kabla mimba yako haijatungwa, hukuwepo. Huo ndio ukweli wa mambo.

      Kwa hiyo, ni jambo linalopatana na akili kuamini kwamba tunarudia hali ileile tuliyokuwa nayo kabla ya kuwa hai. Ni kama tu Mungu alivyomwambia Adamu baada ya kutenda dhambi: “Kwa maana wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.” (Mwanzo 3:19) Wanadamu hawatofautiani na wanyama katika maana hiyo. Hali ya wafu iko kama vile tu Biblia inasema: “Mwanadamu si bora kuliko mnyama.”—Mhubiri 3:19, 20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki