Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwongozo Bora wa Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
    • Andiko la Mhubiri 9:5, 10 linasema hivi: “Wafu, hawajui lolote kamwe . . . Hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika [Sheoli], mahali unapokwenda.” Sheoli ni nini? Ni kaburi ambamo wanadamu huenda wanapokufa. Kaburini, wafu hawafanyi lolote, hawasongi, hawahisi, wala hawafikirii jambo lolote. Ni kana kwamba wanalala usingizi mzito.a Hivyo, Biblia inaonyesha wazi kwamba Mungu hawachukui wapendwa wetu ili wawe pamoja naye huko mbinguni. Kwa sababu ya kifo, wako kaburini bila uhai.

      Yesu alithibitisha ukweli huo baada ya kifo cha rafiki yake Lazaro. Yesu alilinganisha kifo na usingizi. Ikiwa Lazaro alienda mbinguni kuwa pamoja na Mungu Mweza-Yote, halingekuwa jambo la fadhili kwa Yesu kumrudisha duniani ili mwishowe afe tena. Simulizi lililoongozwa kwa roho ya Mungu linasema kwamba kwenye kaburi, Yesu alipaaza sauti hivi: “Lazaro, njoo huku nje!” Biblia inaendelea kusema: “Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka.” Hivyo, Lazaro akawa hai tena. Yesu alijua kwamba Lazaro hakuondoka duniani na kwenda mahali pengine. Alikuwa amelala kaburini akiwa amekufa.—Yohana 11:11-14, 34, 38-44.

  • Mwongozo Bora wa Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Juni 15
    • a Kitabu kimoja (Encyclopædia Britannica, 2003) kinasema kwamba Sheoli ni “mahali ambapo hapana maumivu wala furaha, wala adhabu, wala thawabu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki