-
Wazazi Wetu wa Kale Wako Wapi?Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
-
-
Hali ya Wafu
10. Biblia inasema nini kuhusu hali ya wafu?
10 Hivyo, basi, wafu wako katika hali gani? Kwa kuwa Yehova ndiye aliyewaumba wanadamu, yeye pia anajua kile ambacho hutupata tunapokufa. Neno lake hufundisha kwamba wafu hawana uhai, hawawezi kusikia, kuona, kuongea, wala kufikiria chochote. Biblia inasema:
● “Wafu hawajui neno lo lote.”—Mhubiri 9:5.
● “Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja.”—Mhubiri 9:6.
● “Hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko [kaburini] uendako wewe.”—Mhubiri 9:10.
11. Baada ya Adamu kufanya dhambi, Yehova alimwambia nini?
11 Fikiria yale ambayo Biblia inasema kuhusu mzazi wetu wa kwanza, Adamu. Yehova alimwumba Adamu “kwa mavumbi ya ardhi.” (Mwanzo 2:7) Kama Adamu angalitii sheria ya Yehova, angaliishi milele kwa furaha duniani. Hata hivyo, Adamu alivunja sheria ya Yehova, na adhabu ikawa kifo. Adamu alienda wapi alipokufa? Mungu alimwambia: ‘Utairudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.’—Mwanzo 3:19.
12. Ni nini kilichompata Adamu alipokufa?
12 Adamu alikuwa wapi kabla Yehova hajamwumba kutoka mavumbini? Hakuwapo. Kwa hiyo Yehova aliposema kwamba Adamu ‘angeirudia ardhi,’ Alimaanisha kwamba Adamu angerudi katika hali ya kukosa uhai kama vile mavumbi. Adamu hakuendelea kuishi katika ulimwengu wa roho. ‘Hakuiaga dunia’ kwenda katika makao ya roho ya wazazi wa kale. Hakuenda mbinguni wala motoni. Alirudi katika ile hali ya kutokuwa na uhai; hali ya kutokuwapo.
13. Ni nini huwapata wanadamu na wanyama wanapokufa?
13 Je, jambo hilo huwapata wanadamu kwa ujumla? Ndiyo. Biblia inaeleza: “[Wanadamu na wanyama] huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.”—Mhubiri 3:19, 20.
14. Kuna tumaini gani kwa wafu?
14 Biblia inaahidi kwamba Mungu atawaamsha wafu waishi katika dunia paradiso. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Lakini jambo hilo litatukia wakati ujao. Wakati huu wafu wamelala usingizi wa kifo. (Yohana 11:11-14) Hatupaswi kuwaogopa wala kuwaabudu, kwa kuwa hawawezi kutusaidia wala kutudhuru.
-
-
Wazazi Wetu wa Kale Wako Wapi?Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
-
-
Wafu Hawawezi Kutusaidia
Chifu mmoja maarufu wa Afrika Magharibi alikufa mwaka wa 1990. Alikuwa na wake watano na watoto wengi. Alikuwa anapata pesa nyingi sana kutokana na biashara zake mbili.
Chifu huyo alipokufa, watu wa familia yake walifuata mila za mazishi kwa makini, wakiamini kwamba kwa kufanya hivyo wanaiheshimu roho yake. Wake zake walivaa nguo nyeusi, wakaachilia nywele zao bila kuzichana, wakawa wanakula chakula kidogo, na hawakuoga. Walilia na kuomboleza kwa siku saba baada ya mazishi. Kisha, kupatana na desturi za huko, familia nzima ikakusanyika pamoja na watu wa ukoo katika sherehe ya kula, kunywa, na kucheza dansi ili kumalizia desturi za mazishi.
Kwa kweli, kama chifu huyo aliyekufa angekuwa na uwezo, angeilinda familia yake yenye upendo na kuibariki sana! Lakini hakufanya hivyo. Biashara zake zilifilisika. Watu wa familia yake waligombania mali aliyoacha na baadaye wakatengana. Sasa kumebaki watu wachache sana katika makao makubwa ya chifu huyo ambayo wakati mmoja yalijaa watu.
Wafu Hawawezi Kutudhuru
Katika kijiji fulani nchini Nigeria, mtu mmoja alikufa na kuzikwa. Baadaye, mke wake aliota kwamba mume wake alitaka saa yake. Aliamini ndoto hiyo, hivyo akachukua saa hiyo na kuifukia kando ya mwili wa mume wake.
Mwanamume kijana aitwaye Dunikan aliifukua saa hiyo kisiri na kuitumia miaka mingi hadi ikachakaa. Hakupatwa na jambo lolote baya. Kama mtu huyo aliyekufa angekuwa na uwezo juu ya watu walio hai, bila shaka angemwadhibu mwizi huyo aliyeiba saa yake kutoka kaburini!
Sanduku: Ni mambo gani yaliyoonwa ambayo yanayoonyesha kwamba wafu hawawezi kutusaidia wala kututendea mabaya?
-