-
Isaya Atabiri ‘Tendo la Ajabu’ la YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Viziwi Watasikia”
25. “Viziwi” watasikiaje?
25 Ijapokuwa hivyo, kuna wokovu kwa watu mmoja-mmoja wanaodhihirisha imani. (Soma Isaya 29:17-24; linganisha Luka 7:22.) “Viziwi watasikia maneno ya hicho chuo,” ujumbe ulio katika Neno la Mungu. Naam, huo si uponyaji wa uziwi wa kimwili. Ni uponyaji wa kiroho.
-
-
Isaya Atabiri ‘Tendo la Ajabu’ la YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
26. “Viziwi” leo husikia vikumbusha gani vya kiroho?
26 “Viziwi” hao wanaosikia Neno la Mungu leo hujifunza nini? Wanajifunza kuwa Wakristo wote, hasa wale ambao kutaniko linawaiga wakiwa vielelezo, lazima wajitahidi sana ‘wasikose kwa kileo.’ (Isaya 28:7) Na zaidi, tusichoke kamwe kuvisikia vikumbusha vya Mungu, vinavyotusaidia kuwa na mtazamo wa kiroho kwa mambo yote. Ingawa kwa kufaa Wakristo hujitiisha kwa mamlaka za kiserikali na kuzitegemea ziwaandalie huduma fulani, wokovu huja kutoka kwa Yehova Mungu, wala sio kwa ulimwengu. Pia, hatupaswi kusahau kamwe kwamba, kama vile ilivyokuwa hukumu dhidi ya Yerusalemu lenye kuasi, hukumu ya Mungu dhidi ya kizazi hiki haiepukiki. Kwa msaada wa Yehova, twaweza kuendelea kutangaza onyo lake licha ya upinzani, kama Isaya alivyofanya.—Isaya 28:14, 22; Mathayo 24:34; Waroma 13:1-4.
-