-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
Maswali Yanayohusu Kifo na Maisha Baada ya Kifo
Wakati fulani uliopita, mama ya Karen alikufa. Tangu alipokuwa mtoto, Karen, anayeishi Marekani aliamini kwamba watu wote wema wanapokufa wanaenda mbinguni. Imani hiyo haikumfariji sana. Alijiuliza hivi: ‘Kwa kuwa mama yangu sasa yuko mbinguni, anafananaje? Nitampataje nikifika huko? Je, nitafika huko? Nitakapokufa, je, kuna uwezekano kwamba nitakwenda mahali pengine?’
Karen alianza kujifunza Biblia kwa uangalifu pamoja na Mashahidi wa Yehova. Alijifunza kwamba wafu hawako mbinguni lakini wamelala usingizi mzito. “Hawajui lolote kamwe,” linasema andiko la Mhubiri 9:5. Lakini, je, inawezekana amwone mama yake tena?
Maneno yafuatayo kutoka katika Biblia yalimpa faraja na tumaini: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti [ya Kristo] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29) Karen alijifunza kwamba Mungu wa Biblia kupitia Mwana wake, atawafufua wafu waishi hapahapa duniani. Karen alisema hivi: “Mafundisho ya Biblia yanayohusu kifo na ufufuo yanapatana na akili.”
-
-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
[Picha katika ukurasa wa 23]
Karen, Marekani
-