-
Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kwa mara ya kwanza, Yesu haanzi ujumbe wake kwa neno la pongezi. Badala ya hiyo, yeye anasema: “Na kwa malaika wa kundi katika Sardisi andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo husema yeye ambaye ana roho saba za Mungu na nyota saba, ‘Mimi najua matendo yako, ya kwamba wewe una jina la kwamba wewe u hai, lakini wewe u mfu.’”—Ufunuo 3:1, NW.
-
-
Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lile kundi katika Sardisi lina sifa ya kuwa hai, lenye kutenda. Lakini Yesu anaweza kuona kwamba limekufa kiroho. Kwa wazi, walio wengi wa washiriki walo wamerudia utepetevu unaofanana na hali waliyokuwa nayo kabla ya kuwa Wakristo.—Linga Waefeso 2:1-3; Waebrania 5:11-14.
3. (a) Ni kwa nini imempasa “malaika wa kundi katika Sardisi” aangalie kwa njia maalumu uhakika wa kwamba Yesu ana “nyota saba”? (b) Ni shauri gani kali ambalo Yesu analipa kundi katika Sardisi?
3 Yesu anamkumbusha pia “malaika wa kundi katika Sardisi,” kwamba Yeye ndiye ambaye ana “nyota saba.” Yeye anashika hao wazee wa kundi katika mkono wake wa kulia, akiwa na mamlaka kuwaelekeza katika kazi yao ya kuchunga. Inawapasa wao kuweka mioyo yao katika ‘kujua hakika mwonekano wa kundi.’ (Mithali 27:23, NW) Kwa sababu hiyo, afadhali wasikilize kwa makini maneno ya Yesu yanayofuata: “Uwe mwenye kulinda, na kuimarisha vitu vinavyobaki vilivyokuwa tayari kufa, kwa kuwa mimi sikupata kuona matendo yako yakiwa yamefanywa kwa ukamili mbele za Mungu wangu. Kwa hiyo, endelea kukumbuka jinsi wewe umepokea na jinsi wewe ulisikia, na kuzidi kukishika, na kutubu. Kwa hakika usipoamka, mimi nitakuja kama mwivi, na wewe hutajua hata kidogo ni kwenye saa gani mimi nitakuja juu yako wewe.”—Ufunuo 3:2, 3, NW.
4. Maneno ya Petro yangesaidiaje kundi katika Sardisi “kuimarisha vitu vinavyobaki”?
4 Wazee katika Sardisi wanahitaji kukumbuka ile furaha waliyokuwa nayo kwanza wakati walipojifunza ule ukweli na zile baraka walizopokea wakati huo. Lakini sasa wao ni wafu kwa habari ya utendaji wa kiroho. Taa yao ya kikundi ilikuwa ikiwaka na kuzimika kwa kukosa kazi za imani. Miaka mingi huko nyuma, mtume Petro aliandikia makundi katika Esia (yaelekea kutia na Sardisi) wajenge uthamini kwa ajili ya zile habari njema tukufu ambazo Wakristo walikuwa wamekubali na zilizokuwa zimetangazwa “kwa roho takatifu iliyotumwa kutoka mbinguni”—kama inavyowakilishwa na zile roho saba za njozi ya Yohana. Petro alikumbusha pia Wakristo hao wa Esia kwamba wao walikuwa ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya mali ya pekee, ili wapate kutangaza kotekote sifa bora za mmoja ambaye aliwaita kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’ (1 Petro 1:12, 25; 2 Petro 2:9, NW) Kutafakari juu ya kweli hizo za kiroho kutasaidia kundi katika Sardisi litubu na ‘kuimarisha vitu vinavyobaki.’—Linga 2 Petro 3:9, NW.
5. (a) Ni jambo gani lililoupata uthamini wa Wakristo katika Sardisi? (b) Ni jambo gani litakalotukia ikiwa Wakristo wa Sardisi hawaitikii shauri la Yesu?
5 Kwa wakati uliopo, uthamini na upendo wao kwa ajili ya ukweli ni kama moto ambao karibu umepoa. Ni makaa machache tu yanayoendelea kuwaka. Yesu anawatia moyo wapulize, wachochee moto huo, watubu dhambi ambazo katika hizo uzembe wao umewaongoza, na kuwa kundi hai kiroho tena. (Linga 2 Timotheo 1:6, 7.) La sivyo, wakati Yesu ajapo bila kutazamiwa—“kama mwivi”—kutekeleza hukumu, kundi katika Sardisi litakuwa haliko tayari.—Mathayo 24:43, 44.
Kuja “Kama Mwivi”
6. Yesu alikujaje “kama mwivi” katika 1918, na alikuta hali gani miongoni mwa waliodai kuwa wafuasi wake?
6 Onyo la Yesu kwamba yeye angekuja “kama mwivi” linafika mpaka ndani ya nyakati za ki-siku-hizi. Lilikuwa na tumizi la pekee kwa Wakristo walioishi mpaka kuingia katika siku ya Bwana. Upesi baada ya 1914, kulikuwako utimizo wa unabii wa Malaki: “‘Kwa ghafula Bwana wa kweli atakuja kwenye hekalu Lake, ambaye nyinyi watu mnatafuta, na mjumbe wa agano ambaye katika yeye nyinyi mnapendezwa. Tazama! Yeye atakuja kwa hakika,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Malaki 3:1, NW; Ufunuo 1:10) Akiwa “mjumbe wa agano,” Yesu alikuja kukagua na kuhukumu wale waliodai kuwa wafuasi wake. (1 Petro 4:17) Wakati huo, katika 1918, Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imejitia katika umwagaji-damu katika Vita ya Ulimwengu 1, na ilikuwa mfu kabisa, kiroho. Hata Wakristo wa kweli, ambao kabla ya vita walikuwa wamehubiri kwa bidii, walipitia wakati wa lepe la usingizi wa kiroho. Baadhi ya wazee wao mashuhuri walitiwa gerezani, na utendaji wa kuhubiri ukakaribia kukoma. Wakati roho ya Yehova ilipoamsha Wakristo hawa mwaka uliofuata, si wote waliokuwa tayari. Baadhi yao, kama wale wanawali wapumbavu wa mfano wa Yesu, hawakutayarishwa kwa vifaa kiroho kwa ajili ya pendeleo la kumtumikia Yehova. Hata hivyo, kwa furaha, walikuwako wengi ambao, kama wale wanawali waangalifu, walikuwa wametii onyo la Yesu: “Fulizeni kulinda, basi, kwa sababu nyinyi hamjui wala siku yenyewe wala saa yenyewe.”—Mathayo 25:1-13, NW.
7. Ni kwa nini Wakristo leo wanahitaji kukaa hali wameamka?
7 Uhitaji wa Mkristo kuendelea kuwa chonjo haukumalizika mapema katika siku ya Bwana. Katika unabii wake mkubwa kuhusu “ile ishara wakati mambo yote haya yamekusudiwa kuja kwenye umalizio,” Yesu alitoa onyo lenye mkazo: “Kuhusu siku hiyo au saa hakuna mtu anayejua . . . Fulizeni kutazama, fulizeni kuamka, kwa maana nyinyi hamjui wakati uliowekwa ni lini. Lakini kitu ninachoambia nyinyi ninaambia wote, fulizeni kulinda.” (Marko 13:4, 32, 33, 37, NW) Ndiyo, mpaka saa ii hii, kila mmoja wetu, awe ni wa wapakwa-mafuta au wa ule umati mkubwa, anahitaji kukaa chonjo na kupiga vita dhidi ya kupeperushwa kuingia ndani ya usingizi wa kiroho. Siku ya Yehova ijapo ‘kama mwivi usiku,’ sisi na tupatikane tukiwa tumeamka kabisa ili tupokee hukumu yenye upendeleo.—1 Wathesalonike 5:2, 3; Luka 21:34-36, NW; Ufunuo 7:9.
8. Jamii ya Yohana imechocheaje watu wa Mungu leo wafulize kuwa hai kiroho?
8 Ile jamii ya Yohana leo yenyewe imeamka kuona uhitaji wa kuchochea watu wa Mungu waendelee kuwa hai kiroho. Kwa kusudi hilo, makusanyiko ya pekee hupangwa kotekote duniani mara kadhaa kila mwaka. Katika mwaka mmoja wa majuzi, hadhirina kwenye mikusanyiko ya wilaya 2,981 ilijumlika kuwa 10,953,744, na waumini wapya 122,701 wakabatizwa. Kwa zaidi ya miaka mia moja, ile jamii ya Yohana imetumia gazeti Mnara wa Mlinzi katika kutangaza jina na kusudi la Yehova. Katika kuitikia minyanyaso mikali wakati wa vile vita viwili vya ulimwengu, Mnara wa Mlinzi uliwaamsha Mashahidi wa Yehova kwenye bidii mpya kwa kutangaza makala kama vile “Wabarikiwa ni Wasioogopa” (1919), “Mwito Kwenye Tendo” (1925), na “Kushindwa kwa Mnyanyaso” (1942).
9. (a) Imewapasa Wakristo wote wawe wakijiuliza wenyewe nini? (b) Ni kitia-moyo gani kimetolewa na Mnara wa Mlinzi?
9 Kama vile katika Sardisi, ndivyo ilivyo katika makundi leo, uchunguzi mwendelevu wa kibinafsi ni wa muhimu kwa Wakristo wote. Sisi sote inatupasa tuendelee kujiuliza wenyewe: Je! ‘matendo yetu yamefanywa kikamili’ mbele za Mungu wetu? Bila ya kuhukumu wengine, je! sisi kibinafsi tunasitawisha ile roho ya kujidhabihu na kujitahidi kutoa utumishi wa nafsi yote kwa Mungu? Kuhusiana na hili gazeti Mnara wa Mlinzi limetoa kitia-moyo kwa kuzungumzia habari kama vile “Endeleeni Kuthibitisha Ninyi Wenyewe Jinsi Mlivyo” na “Kuishi Si kwa Ajili Yetu Wenyewe Tena.”a Tukiwa na misaada kama hiyo ya Kimaandiko, acheni sisi tuchungue utu wetu wa ndani-ndani zaidi tunapojaribu kutembea kwa unyenyekevu na kwa sala katika ukamilifu mbele za Yehova.—Zaburi 26:1-3; 139:23, 24.
-