Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Imarisha Tumaini Lako Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Juni 1
    • Tunaweza kufanya nini tunapokabiliwa na hali hizo? Ingawa ni jambo la kawaida kuogopa uhai wako unapohatarishwa, twaweza kukumbuka maneno yenye kutia-moyo ya mtume Paulo: “[Yehova] amesema: ‘Hakika sitakuacha kwa vyovyote wala kukuachilia mbali kwa vyovyote.’ Ili kwamba tupate kuwa wenye moyo mkuu na kusema: ‘Yehova ni msaidiaji wangu; hakika sitaogopa. Mwanadamu aweza kunifanya nini?’” (Waebrania 13:5, 6) Twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova huhisi vivyo hivyo kuelekea watumishi wake leo. Hata hivyo, kujua ahadi za Yehova si sawa na kuwa na uhakikisho kwamba atatenda kwa niaba yetu. Kwa hiyo ni muhimu sana tuchunguze msingi wa kujenga tumaini katika Yehova na kuhakikisha kwamba tunafanya yote tuwezayo kuimarisha na kudumisha tumaini hilo. Tukifanya hivyo, “amani ya Mungu izidiyo fikira yote kwa ubora italinda mioyo [yetu] na nguvu [zetu] za akili kwa njia ya Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:7) Kisha majaribu yatokeapo, tutaweza kufikiri ifaavyo na kukabiliana nayo kwa hekima.

  • Imarisha Tumaini Lako Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Juni 1
    • Kwa kuwa Yehova Mungu ni Mweza Yote, bila shaka anaweza kuwalinda watumishi wake chini ya hali zozote zile. (Isaya 33:22; Ufunuo 4:8) Lakini hata wakati ambapo Yehova huruhusu baadhi ya watumishi wake wathibitishe uaminifu wao hadi kifo, bado huwategemeza na kuwasaidia wadumishe uaminifu-maadili wao, akiwawezesha wadumu wakiwa imara, wenye shangwe, na wenye utulivu hadi mwisho. Kwa hiyo, twaweza kuwa na uhakika kama mtunga-zaburi: “Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.”—Zaburi 46:1, 2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki